MAJUKWAA ya wanaume yatumike kupinga Ukatili wa Kijinsia | The Dodoma Post
The Dodoma Post Watoto

MAJUKWAA ya wanaume yatumike kupinga Ukatili wa Kijinsia

WANAHARAKATI wa kifeminia nchini wametakiwa kujikita katika kuelimisha kuhusu ulinzi wa mtoto wa kiume kwa mustakabali wa haki na usawa wa jinsia.

Florah Amon
By Florah Amon
07 Nov 2023
MAJUKWAA ya wanaume yatumike kupinga Ukatili wa Kijinsia

Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 11 ,2023 jijini Dar es salaam, na  MAKAMU wa Rais Mstaafu wa Afrika Kusini,  Phumzile Mlambo  Ngcuka katika tamasha la jinsia la 15 pamoja na kuadhimisha  miaka 30 ya taponla kifeminia la Mtandao wa jinsia nchini (TGNP).

Phumzile  amesema kuwa  ipo haja ya kuwa na majukwaa ya wanaume nchini yenye kueleza yanayowahusu lakini pia  yakitumika kuchukua hatua za kupinga ukatili wa kijinsia, wanaopinga ubaguzi  dhidi ya wanawake na  wanaokataa ndoa za utotoni.

Ameongeza kuwa katika harakati za kukataa ukandamizaji wa aina yoyote  pia suala la ulinzi wa mtoto wa kiume halina budi kuzingatiwa kaa kuendeleza ajenda za kumkomboa.

"Wanaharakati wa haki za binadamu wasiruhusu aina yoyote ya ukatili  kuanzia kuukataa  mfumo dume kuanzia katika ngazi ya familia," amesema Phumzile.

Aidha amesema  mfumo dume sio rafiki kwa wanawake na hata wanaume  na  umekuwa  ukiendeleza  ubaguzi hivyo ni muhimu kwa wanaume na watoto wankiumenkuwa miongoni mwa harakati za kuupinga  kwani kaa karne hii inahitaji wanaume wenye mshikamano  na wenza wao.

Kwa upande wake , Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP, Gema Akilimali alisema  licha ya Mtandao huo  kuadhimisha miaka 15 za usawa wa kijinsia lakini  changamoto bado ni nyingi na mshikamano na serikali unahitajika zaidi kwa sasa kuliko huko walikotoka.

Amesema katika  tamasha hilo la siku nne watatoka na maazimio ya jumla  kwani upo mchango wa TGNP katika harakati mbalimbali.

Lilian Liundi ni  Mkurugenzi Mtendaji wa TNGP,  ambapo amesema  Tamasha la jinsia  ni jukwaa la kuleta sauti kwa pamoja lenye kujadili kwa pamoja na kupanga  mikakati.

"Tamasha hili ni la 15 tangu kuanzishwa  limeweza kuwa na washiriki 2000 hadi 5000 kwa tamasha moja limewafikia watu zaidi ya 35000,"amesema Liundi.

Amesema tamasha hilo limewaleta watu kwa pamoja ukanda wa Afrika na wameendelea kusimama kwenye misingi ya wasisi wao.

Aidha ameongeza kuwa  TGNP imejengwa katika  misingi imara  ya haki na kuondoa mifumo kandamizi.
 

JESHI la polisi linawashikilia watu 121 huku 1 kati yao akitekeleza mauaji ya mtoto wa kiume.

JESHI la polisi linawashikilia watu 121 huku 1 kati yao akitekeleza mauaji ya mtoto wa kiume.

WATANZANIA Wote lazima kufika sekondari kwa asilimia 100.

WATANZANIA Wote lazima kufika sekondari kwa asilimia 100.

KONGAMANO lawakutanisha Wanafunzi, wafanyakazi na Wastaafu wa IRDP Kuelekea Mahafari ya 37

KONGAMANO lawakutanisha Wanafunzi, wafanyakazi na Wastaafu wa IRDP Kuelekea Mahafari ya 37

CHUO cha Mwalimu Nyerere kuleta Neema Butiama

CHUO cha Mwalimu Nyerere kuleta Neema Butiama

TEHAMA Kutoa Mafunzo kwa Wataalamu 500

TEHAMA Kutoa Mafunzo kwa Wataalamu 500