TEHAMA Kutoa Mafunzo kwa Wataalamu 500 | The Dodoma Post
The Dodoma Post Watoto

TEHAMA Kutoa Mafunzo kwa Wataalamu 500

Katika moja ya Vipaumbele vya Tume kwa mwaka wa fedha 2023/24 inatarajiwa kuwezesha mafunzo maalum ya wataalam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) 500 ili kukuza na kuendeleza ujuzi wa teknolojia hiyo nchini.

Winner Marawiti
By Winner Marawiti
25 Aug 2023
TEHAMA Kutoa Mafunzo kwa Wataalamu 500

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo nchini Dkt. Nkundwe Mwasaga wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu utekelezaji wa Majukumu na mwelekeo wa Tume hiyo leo Jijini Dodoma na kusema kukuza soko la bidhaa na huduma za kampuni ndogondogo “startup” kwa kushiriki maonesho na makongamano yanayohusu fursa za startups duniani.

''Kuratibu na kutengeneza mfumo wa usimamizi wa utekelezaji wa Sera ya TEHAMA na kufanya tafiti za kuweza kufanya maboresho ya sera kulingana na mabadiliko ya teknolojia,'' amesema Dkt. Mwasaga

Aidha amebainisha Mafanikio ya Tume kwa mwaka 2022/23  ambapo amesema wamefanikiwa kutengeneza mfumo jumuishi utakaounganisha usajili na uendelezaji wa wataalam na wabunifu TEHAMA nchini.

‘’Lengo la mfumo huu ni kutambua bunifu na kupanua wigo wa ukuzaji wa wabunifu na bidhaa na huduma za TEHAMA zinazozalishwa Tanzania na hivyo kukuza pato la Taifa na kuongeza fursa za ajira kupitia TEHAMA na maendeleo ya kidijitali duniani,'' amesema Dkt. Mwasaga

Kwa upande wake Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amesema Serikali imeamua kuwekeza kwa nguvu kwenye Tanzania ya Kidijitali chini ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambapo msimamizi mkuu unafanywa na Tume ya TEHAMA.

JESHI la polisi linawashikilia watu 121 huku 1 kati yao akitekeleza mauaji ya mtoto wa kiume.

JESHI la polisi linawashikilia watu 121 huku 1 kati yao akitekeleza mauaji ya mtoto wa kiume.

WATANZANIA Wote lazima kufika sekondari kwa asilimia 100.

WATANZANIA Wote lazima kufika sekondari kwa asilimia 100.

KONGAMANO lawakutanisha Wanafunzi, wafanyakazi na Wastaafu wa IRDP Kuelekea Mahafari ya 37

KONGAMANO lawakutanisha Wanafunzi, wafanyakazi na Wastaafu wa IRDP Kuelekea Mahafari ya 37

CHUO cha Mwalimu Nyerere kuleta Neema Butiama

CHUO cha Mwalimu Nyerere kuleta Neema Butiama

MAJUKWAA ya wanaume yatumike kupinga Ukatili wa Kijinsia

MAJUKWAA ya wanaume yatumike kupinga Ukatili wa Kijinsia