

Maandalizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yanaendelea kushika kasi hasa kwenye ujenzi wa miundombinu ili kuhakikisha kila kitu cha lazima kwenye mashindano hayo kinakuwa tayari kwaajili ya kutumika ifikapo 2027.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro alitembelea mradi wa ujenzi wa kiwanja kipya cha Dkt. Samia Suluhu Hassan August 29, 2024, kiwanja kinachoendelea kujengwa jijini Arusha.
Akiwa huko, Dkt. Ndumbaro aliwaomba wakandarasi wa mradi huo kufanya kazi kwa weledi na ufanisi huku akiwahakikishia kufika katika eneo hilo kwaajili ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi kila baada ya wiki mbili.
“Matarajio yetu ni kwamba mkandarasi atafanya kazi kwa wakati na atakabidhi mradi kwa wakati, tumeshamwambia mshauri mwelekezi ya kwamba amsimamie vizuri mkandarasi ili kazi iwe na ubora sana na amalize kwa wakati,” amesema Dkt. Ndumbaro.
Ujenzi wa uwanja huo umefikia asilimia tano katika hatua ya awali ukihusisha uandaaji wa eneo la uwanja, manunuzi na ujenzi wa ofisi za mkandarasi.
“Uwanja huo ni maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, alishasema nataka Tanzania kwa kushirikiana na nchi wenyeji Kenya na Uganda kuwa wenyeji wa mashindano ya Afcon 2027, maono yale ndiyo yamezaa mradi huu, tungekosa kuwa wenyeji sidhani kama mradi huu ungekuwepo leo,” ameongeza Dkt. Ndumbaro.
Waziri Dkt. Ndumbaro amewahakikisha wakazi wa Arusha kupata ajira za muda wakati wa ujenzi wa mradi huo, ikiwa ni sehemu ya kuwanufaisha wenyeji huku akiamini kuwa ujenzi utazingatia viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA).
“Kwa wana Arusha mradi huu ni muhimu sana kwenu, umekuja nyumbani kwenu tushirikiane na serikali katika kuhakikisha unakwenda vizuri, nimefanya maongezi na Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda naye ameniahidi atausimamia kwa karibu zaidi kwa sababu yeye yuko Arusha muda wote,” amesema Dkt. Ndumbaro.
Uwanja huo unaojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 286 utakuwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 30,000, vyumba vya watu mashuhuri, sehemu ya makumbusho na huduma nyingine ambazo zitaufanya utumike kila siku.
BODI YA MKONGE TANZANIA YATANGAZA FURSA KWA WATANZANIA.
SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.
DCEA:SERIKALI IMEPUNGUZA KASI YA WALAIBU WA DAWA ZA KULEVYA.
ULINZI NA USALAMA BAHARINI UMEIMARIKA;TASAC
VITONGOJI VYOTE 64,359 VITAKUWA NA UMEME IFIKAPO 2030
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.
Mkoa wa Katavi umeendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM)
UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.
AMANZI NA BABU TALE USO KWA USO JIMBONI