Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661 | The Dodoma Post
The Dodoma Post Makala

Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661

Sekta ya Uvuvi ni miongoni mwa Sekta za uzalishaji ambayo inatoa ajira za moja kwa moja kwa wavuvi 201,661, wakuzaji viumbe maji 49,084 na takriban watanzania milioni 6 wanajishughulisha na kazi mbalimbali zinazohusiana na uvuvi katika mnyororo wa thamani.

Moreen Rojas (Dodoma)
By Moreen Rojas (Dodoma)
06 May 2025
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja  Kwa Wavuvi 201,661

Hayo yameelezwa Mei 6 2025 jijini hapa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dkt, Ashatu Kijaji wakati akieleza mafanikio ya Miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan katika ukumbi wa Idara Maelezo.

Hali ya uzalishaji wa mazao ya uvuvi umeongezeka kutoka tani 477,018.84,zenye thamani ya shilingi2,775,798,531.30 katika mwaka 2021, hadi kufikia tani 522,788.33,zenye thamani ya shilingi4,352,735,640.54,katika mwaka 2024.

Aidha, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2024, jumla ya tani 1,951,296.33 za mazao ya uvuvi, zenye thamani ya shilingi 13,647,504,498.08, zilizalishwa kutoka katika maji ya asili.

Serikali imeendelea kuimarisha biashara ya mazao ya uvuvi katika soko la ndani na nje ya nchi ambapo, mauzo ya mazao ya uvuvi na samaki hai wa mapambo yameongezeka kutoka tani 42,302.03za mazao ya uvuvi na samaki hai wa mapambo 181,268zenye thamani ya dola za Marekani 457,817,845,082 kwa mwaka 2021 hadi kufikia tani 59,746.41 za mazao ya uvuvi na samaki hai wa mapambo 148,041zenye thamani ya shilingi 752,969,498,996 mwaka 2024.

"Hivyo, Ongezeko hili limetokana na kuboreshwa kwa mazingira ya biashara ikiwa ni pamoja kufanya mauzo ya mazao ya uvuvi kuongezeka hadi kufikia tani 181,655.7 na samaki hai wa mapambo 729,413 yenye thamani ya shilingi 2,282,092,677,530. na kupungua kwa baadhi ya tozo na kuimarika kwa masoko ya mazao nje ya nchi"

Aidha, ongezeko la thamani ya samaki hai wa mapambo limetokana na kuimarika kwa soko la samaki hai nchi za nje zikiwemo nchi za Poland, Denmark, Ujerumani, Marekani na Uswisi.

Serikali imeendelea na ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko ambapo hadi kufikia Aprili, 2025 ujenzi huo umefikia asilimia 81.9 na unatarajiwa kukamilika Mwezi Juni mwaka 2025. Mradi huu una thamani ya shilingi bilioni 279.5

Ujenzi huo umejumuishaJengo la kuzalishia barafu, kuhifadhia, kuandalia samaki pamoja na soko la kuuzia samaki; Kituo cha kusambazia maji safi; Kituo cha zimamoto; Kituo cha kupoozea umejumuisha:Ujenzi wa gati lenye urefu wa mita za mraba 315;Jengo la utawala; umeme; Kituo cha kuzalishia gesi ya naitrojeni; Sehemu ya kuegesha magari;Tanki za kuhifadhia mafuta;na karakana ya kutengenezea meli.

Aidha, kukamilika kwa kuchochea uwekezaji katika ujenzi wa viwanda vya kuchakata samaki na miundombinu ya uhifadhi wa mazao ya uvuvi,Pia, meli hizo zitatia nanga kupata na kushusha samaki wanaolengwa na wale wasiolengwa hivyo,Bandari hiyo,pamoja na masuala mengine kutawezesha meli za uvuvi zinazovua mazao ya uvuvi katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari yaTanzania (EEZ) na Bahari huduma mbalimbali za kijamii kutoka kwa wafanyabiasha wa ndani ya nchi,Vile vile, jumla ya wananchi 570 wamepata ajira ya moja kwa moja kupitia mradi huu.

Aidha Mwenendo wa uzalishaji wa samaki na viumbe maji wengine katika maji ya asili duniani unaonesha kupungua ukilinganisha na mwenendo wa kuongezeka kwa mahitaji ya samaki na mazao mengine ya ukuzaji viumbe maji.

Washirika wa Maendeleo na Sekta Binafsi umewezesha uzalishaji wa mazao ya ukuzaji viumbe maji kuongezeka kutoka tani 44,735.32 
mwaka 2020/2021 hadi tani 124,024.224 mwaka 2024/2025

Vilevile, uzalishaji wa chakula Cha samakikutoka tani 1,182.47 mwaka 2020/2021na kufanya jumla ya tani 123,346.86 ya chakula cha samaki nchini umeongezeka hadi tani 13,859kwa mwaka 2024/2025zilizozalishwa kwa kipindi husika.

Watumishi wa Bodi ya maziwa waaswa kuzingatia weledi katika kazi zao.

Watumishi wa Bodi ya maziwa waaswa kuzingatia weledi katika kazi zao.

Afcon 2027 Yachochea uendelezwaji wa Makuyuni Wildlife Park

Afcon 2027 Yachochea uendelezwaji wa Makuyuni Wildlife Park

Dkt. Ndumbaro: Nitatembelea Mradi Huu Kila Baada ya Wiki Mbili

Dkt. Ndumbaro: Nitatembelea Mradi Huu Kila Baada ya Wiki Mbili

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027-2

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027-2

MTAALA MPYA WA ELIMU WAANZA KUTUMIKA (MUHAS)

MTAALA MPYA WA ELIMU WAANZA KUTUMIKA (MUHAS)