BRELA Yawasogezea Huduma Wakazi wa Dodoma Wiki Ya Utumishi wa Umma. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Makala

BRELA Yawasogezea Huduma Wakazi wa Dodoma Wiki Ya Utumishi wa Umma.

Wakala wa Usajili wa biashara na Leseni(BRELA) yawaita wakazi wa Dodoma na Mikoa jirani kujitokeza kwa wingi kufika katika Banda lao ili kupata Elimu ya usajili wa biashara na leseni.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
18 Jun 2025
BRELA Yawasogezea Huduma Wakazi wa Dodoma Wiki Ya Utumishi wa Umma.

Hayo yamesemwa na Afisa Leseni Mwandamizi Koyan Abubakari kutoka Brela wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma  yanayoendelea katika viwanja vya Chinangal Park Jijini Dodoma.

Abubakar amesema lengo la Brela kushiriki katika wiki ya Utumishi wa Umma ni kusogeza huduma na kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kujua majukumu ya Brela na kusajili biashara pamoja na kupewa leseni za biashara zao.

"Huduma tunazozitoa  ni kusajili leseni ya  biashara,Kusajili majina ya biashara,Kusajili  viwanda vidogo,Usajili wa alama za biashara ambapo kusajili jina la biashara ni Tsh.20,000 ili mfanyabiashara aweze kufanya majukumu yake bila bugdha."Amesema Abubakar.

Ameongeza kuwa, BRELA imefanikiwa kuongeza mapato kupitia huduma bora kwa wateja na upanuzi wa wigo wa usajili wa biashara na leseni nchini.

Ongezeko la gawio kwa mwaka wa fedha 2024/2025 unatokana na huduma za usajili ambapo hadi kufikia Aprili 2025, BRELA imesajili Kampuni 13,794, Majina ya biashara 23,644, Leseni za Biashara kundi “A” 17,595, Leseni za Viwanda 298, Hataza 37, Alama za Biashara na Huduma 2601. Hiyo ni ishara ya kuimarika kwa uendeshaji wa taasisi na mchango wake kwa maendeleo ya taifa.

Kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo, BRELA imechangia gawio la wastani wa Shilingi bilioni 16.8 kila mwaka na hivyo kutambuliwa rasmi kwa kupewa tuzo ya taasisi bora katika utoaji wa gawio kwa Serikali.

Kwa upande wake mmoja wa wananchi aliyepata huduma katika Banda la Brela Bi  Nzurika Zavala ambaye ni mjasiriamali ameishukuru Brela kwa kumpatia huduma nzuri ambapo anasema amepata ushirikiano tofauti na ulivyotarajia.

"Nimepata ushirikiano mzuri na tayari nimepewa cheti changu mwanzo nilidhani nitasumbuliwa kuwa Rudi baada ya siku kadhaa" amesema Nzurika.

Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja  Kwa Wavuvi 201,661

Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661

Watumishi wa Bodi ya maziwa waaswa kuzingatia weledi katika kazi zao.

Watumishi wa Bodi ya maziwa waaswa kuzingatia weledi katika kazi zao.

Afcon 2027 Yachochea uendelezwaji wa Makuyuni Wildlife Park

Afcon 2027 Yachochea uendelezwaji wa Makuyuni Wildlife Park

Dkt. Ndumbaro: Nitatembelea Mradi Huu Kila Baada ya Wiki Mbili

Dkt. Ndumbaro: Nitatembelea Mradi Huu Kila Baada ya Wiki Mbili

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027-2

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027-2