Mahakama Kenya yaagiza kuzuiliwa kwa akaunti za Mchungaji Ezekiel | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kimataifa

Mahakama Kenya yaagiza kuzuiliwa kwa akaunti za Mchungaji Ezekiel

Mahakama nchini Kenya imeagiza kuzuiliwa kwa akaunti 15 za benki zinazomilikiwa na mchungaji mwenye Ezekiel Odero kwa siku 30.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
08 May 2023
Mahakama Kenya yaagiza kuzuiliwa kwa akaunti za Mchungaji Ezekiel

Mahakama nchini Kenya imeagiza kuzuiliwa kwa akaunti 15 za benki zinazomilikiwa na mchungaji mwenye Ezekiel Odero kwa siku 30, hii inafuatia maombi yaliyowasilishwa na Ofisi ya Mkurungenzi mkuu wa upelelesji wa Mashitaka (DCI) kutaka akaunti zote zizuiliwe wakati uchunguzi ukiendelea.

Katika waraka uliowasilishwa mahakamani, DCI, ilidai Mchungaji Ezekiel wa Kanisa la New Life Prayer Centre anashukiwa kwa utakatishaji wa pesa kutokana na uhusiano na Mchungaji Paul Mackenzie wa Kanisa la Good News International, ambaye anachunguzwa kwa madai ya kuwalaghai wafuasi wa kanisa lake kufunga hadi kufa ili kukutana na Yesu.

Wapelelezi waliiambia mahakama kuwa akaunti za benki za Mchungazji zimekuwa zikipokea kiasi kikubwa cha pesa ambazo pesa zake zinashukiwa kuwa haramu zilizotoka kwa waathirika ambao wanadaiwa kulaghaiwa kuuza mali zao na kumpatia mchungani Mackenzie.

Wameitaka mahakama kuwaruhusu kuzifikia akaunti kadhaa za benki katika Equity Bank, Co-op Bank, KCB na HFC Bank.

Kulingana na ofisa ya polisi wanaofanya uchunguzi ofisi ya DCI, Martin Munene, wanahofu kuwa pesa zilizoshikiliwa katika akaunti mbali mbali za benki zitahamishwa iwapo mahakama haitatoa agizo la kuzuia akaunti hizo.

Wiki iliyopita mchungaji Ezekiel alikwenda katika Mahakama ya juu zaidi mjini Mombasa akitaka kuzuia kufujwa kwa akaunti zake.

Mchungaji Ezekiel alikuwa amedai kuwa kushikiliwa kwa akaunti zake kutakuwa ni kuingilia uhuru wake na wa kanisa waumini wa kanisa lake.

Suala hilo inatarajiwa kuendelea kusikilizwa Jumanne mahakamani, 

Trump Alizuia Israel Isimshambulie Kiongozi wa Iran

Trump Alizuia Israel Isimshambulie Kiongozi wa Iran

ISRAEL yaishambulia Syria, kadhaa wahofiwa kupoteza maisha

ISRAEL yaishambulia Syria, kadhaa wahofiwa kupoteza maisha

MAKAMPUNI MENGI YA KIGENI YANAHITAJI MAFUNDI WENYE UJUZI UNAOKUBALIKA KIMATAIFA.

MAKAMPUNI MENGI YA KIGENI YANAHITAJI MAFUNDI WENYE UJUZI UNAOKUBALIKA KIMATAIFA.

"Historia Itawahukumu Viongozi wa EAC na SADC Kama Watakaa Kimya Kuhusu Mzozo wa Congo"

"Historia Itawahukumu Viongozi wa EAC na SADC Kama Watakaa Kimya Kuhusu Mzozo wa Congo"

"Mzozo wa Ardhi Nchini Afrika Kusini: Trump Afunga Msaada wa Kifedha Kufuatia Sheria ya Unyakuzi wa Ardhi"

"Mzozo wa Ardhi Nchini Afrika Kusini: Trump Afunga Msaada wa Kifedha Kufuatia Sheria ya Unyakuzi wa Ardhi"