

Ikiwa ni mara ya pili tangu Sheikh Ponda Issa Ponda alipotangaza kujiunga na Chama cha ACT WAZALENDO,Umati wa wananchi wahudhuria hadhara ya kisiasa iliyoandaliwa na Chama hicho June,18 2025 iliyofanyika katika viwanja vya Bakharesa Manzese jijini Dar es salaam
Ikiwa ni mara ya pili tangu Sheikh Ponda Issa Ponda alipotangaza kujiunga na Chama cha ACT WAZALENDO,Umati wa wananchi wahudhuria hadhara ya kisiasa iliyoandaliwa na Chama hicho June,18 2025 iliyofanyika katika viwanja vya Bakharesa Manzese jijini Dar es salaam
Akizungumza mbele ya wananchi na waandishi wa habari Sheikh Ponda ameeleza namna watanzania wanavyoweza kuleta mabadiliko makubwa endapo watashiriki kikamilifu katika zoezi la kupiga kura,
"Tunachokifanya sisi ni kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kusimama na kuwa tayari kupiga kura na kulinda kura kwa sababu wabunge wote wa vyama vya upinzani wanaoingia bungeni ulitumika misuli ya wananchi katika kuhakikisha kwamba yule anayepata ridhaa ya wananchi ndiye anayetangazwa"
Pia amebainisha baadhi ya changamoto katika sekta ya afya hususan gharama kubwa wanazotoa waathirika wa magonjwa ya figo katika zoezi la kusafisha damu
"Ndugu zangu hakuna ubinadamu katika eneo la sekta ya afya,mtu figo zake zikifeli anatakiwa kutoa 180000 mara tatu kwa wiki na asipotoa anaambiwa arudi nyumbani matokeo yake mgonjwa anakufa kizembe"
Katika hatua nyingine Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Isihaka Mchinjite ameuhamasisha umma kuungana ili kuleta matokeo chanya katika nchi
Aidha Naibu Katibu Mkuu Bw Ado Shaibu alihitimisha kwa kubainisha lengo la kuanza kufanya hadhara zao katika mkoa wa Dar es Salam ikiwa ni kwa kuwa Jiji la Dar es salaam ni kitovu cha mikosa yote hapa nchini hivyo wanaamini zitaleta matokeo makubwa.
KIHENZILE: UWAZI NA UWAJIBIKAJI NI NGUZO MUHIMU ZENYE TIJA KWA WANANCHI
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.
CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.
ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU
VIJANA WANAOTUMIA VIBAYA MITANDAO YA KIJAMII WAONYWA.
VIONGOZI WAANZA KUWAOGOPA WAJUMBE MOROGORO.
DODOMA YAELEKEA IRINGA KWA KISHINDO MASHINDANO YA UMISSETA.
Serikali Yatangaza Kuanza Msako Kuwabaini Wanaotumikisha Watoto
TANZANIA KUWA MWENYEJI TUZO ZA 32 ZA KIMATAIFA ZA UTALII.