ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM

Ikiwa ni mara ya pili tangu Sheikh Ponda Issa Ponda alipotangaza kujiunga na Chama cha ACT WAZALENDO,Umati wa wananchi wahudhuria hadhara ya kisiasa iliyoandaliwa na Chama hicho June,18 2025 iliyofanyika katika viwanja vya Bakharesa Manzese jijini Dar es salaam

Ngonise Kahise
By Ngonise Kahise
19 Jun 2025
ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM

Ikiwa ni mara ya pili tangu Sheikh Ponda Issa Ponda alipotangaza kujiunga na Chama cha ACT WAZALENDO,Umati wa wananchi wahudhuria hadhara ya kisiasa iliyoandaliwa na Chama hicho June,18 2025 iliyofanyika katika viwanja vya Bakharesa Manzese jijini Dar es salaam

Akizungumza mbele ya wananchi na waandishi wa habari Sheikh Ponda ameeleza namna watanzania wanavyoweza kuleta mabadiliko makubwa endapo watashiriki kikamilifu katika zoezi la kupiga kura,

   "Tunachokifanya sisi ni kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kusimama na kuwa tayari kupiga kura na kulinda kura kwa sababu wabunge wote wa vyama vya upinzani wanaoingia bungeni ulitumika misuli ya wananchi katika kuhakikisha kwamba yule anayepata ridhaa ya wananchi ndiye anayetangazwa"

Pia amebainisha baadhi ya changamoto katika sekta ya afya hususan gharama kubwa wanazotoa waathirika wa magonjwa ya figo katika zoezi la kusafisha damu

 "Ndugu zangu hakuna ubinadamu katika eneo la sekta ya afya,mtu figo zake zikifeli anatakiwa kutoa 180000 mara tatu kwa wiki na asipotoa anaambiwa arudi nyumbani matokeo yake mgonjwa anakufa kizembe"

Katika hatua nyingine Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Isihaka Mchinjite ameuhamasisha umma kuungana ili kuleta matokeo chanya katika nchi

Aidha Naibu  Katibu Mkuu Bw Ado Shaibu alihitimisha kwa kubainisha lengo la kuanza kufanya hadhara zao katika mkoa wa Dar es Salam ikiwa ni kwa kuwa Jiji la Dar es salaam ni kitovu cha mikosa yote hapa nchini hivyo wanaamini zitaleta matokeo makubwa.

KIHENZILE: UWAZI NA UWAJIBIKAJI NI NGUZO MUHIMU ZENYE TIJA KWA WANANCHI

KIHENZILE: UWAZI NA UWAJIBIKAJI NI NGUZO MUHIMU ZENYE TIJA KWA WANANCHI

CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.

CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.

Serikali Yatangaza Kuanza Msako Kuwabaini Wanaotumikisha Watoto

Serikali Yatangaza Kuanza Msako Kuwabaini Wanaotumikisha Watoto

VIJANA WANAOTUMIA VIBAYA MITANDAO YA KIJAMII WAONYWA.

VIJANA WANAOTUMIA VIBAYA MITANDAO YA KIJAMII WAONYWA.

VIONGOZI WAANZA KUWAOGOPA WAJUMBE MOROGORO.

VIONGOZI WAANZA KUWAOGOPA WAJUMBE MOROGORO.