ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM

Ikiwa ni mara ya pili tangu Sheikh Ponda Issa Ponda alipotangaza kujiunga na Chama cha ACT WAZALENDO,Umati wa wananchi wahudhuria hadhara ya kisiasa iliyoandaliwa na Chama hicho June,18 2025 iliyofanyika katika viwanja vya Bakharesa Manzese jijini Dar es salaam

Ngonise Kahise
By Ngonise Kahise
19 Jun 2025
ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM

Ikiwa ni mara ya pili tangu Sheikh Ponda Issa Ponda alipotangaza kujiunga na Chama cha ACT WAZALENDO,Umati wa wananchi wahudhuria hadhara ya kisiasa iliyoandaliwa na Chama hicho June,18 2025 iliyofanyika katika viwanja vya Bakharesa Manzese jijini Dar es salaam

Akizungumza mbele ya wananchi na waandishi wa habari Sheikh Ponda ameeleza namna watanzania wanavyoweza kuleta mabadiliko makubwa endapo watashiriki kikamilifu katika zoezi la kupiga kura,

   "Tunachokifanya sisi ni kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kusimama na kuwa tayari kupiga kura na kulinda kura kwa sababu wabunge wote wa vyama vya upinzani wanaoingia bungeni ulitumika misuli ya wananchi katika kuhakikisha kwamba yule anayepata ridhaa ya wananchi ndiye anayetangazwa"

Pia amebainisha baadhi ya changamoto katika sekta ya afya hususan gharama kubwa wanazotoa waathirika wa magonjwa ya figo katika zoezi la kusafisha damu

 "Ndugu zangu hakuna ubinadamu katika eneo la sekta ya afya,mtu figo zake zikifeli anatakiwa kutoa 180000 mara tatu kwa wiki na asipotoa anaambiwa arudi nyumbani matokeo yake mgonjwa anakufa kizembe"

Katika hatua nyingine Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Isihaka Mchinjite ameuhamasisha umma kuungana ili kuleta matokeo chanya katika nchi

Aidha Naibu  Katibu Mkuu Bw Ado Shaibu alihitimisha kwa kubainisha lengo la kuanza kufanya hadhara zao katika mkoa wa Dar es Salam ikiwa ni kwa kuwa Jiji la Dar es salaam ni kitovu cha mikosa yote hapa nchini hivyo wanaamini zitaleta matokeo makubwa.

CHIPUKIZI ACHUKUA FOMU YA UDIWANI KATA YA MWEMBESONGO.

CHIPUKIZI ACHUKUA FOMU YA UDIWANI KATA YA MWEMBESONGO.

Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum

Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum

DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA

DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA

Katimba aomba ridhaa Ubunge viti maalumu Kigoma

Katimba aomba ridhaa Ubunge viti maalumu Kigoma

SAGAFF AJITOSA KUMRITHI MAVUNDE DODOMA MJINI

SAGAFF AJITOSA KUMRITHI MAVUNDE DODOMA MJINI