TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.

Shirika la umeme nchini TANESCO limeanza rasmi kampeni maalum ya kuhamasisha ulipaji wa madeni kwa wateja wa malipo ya baada lakini pia ukaguzi wa mita za luku kwa wateja wa malipo ya kabla.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
19 Jun 2025
TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.

Shirika la umeme nchini TANESCO limeanza rasmi kampeni maalum ya kuhamasisha ulipaji wa madeni kwa wateja wa malipo ya baada lakini pia ukaguzi wa mita za luku kwa wateja wa malipo ya kabla.

Akizungumza na waandishi wa habari leo juni 19,2025 Jijini Dar es salaam kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na huduma kwa wateja Irene Gowele amesema kampeni hiyo imeanza rasmi leo Juni 19,2025 ambayo imepewa jina la 'lipa deni,linda miundombinu tukuhudumie' ambapo kauli mbiu ya kampeni hiyo ikiwa 'huduma endelevu huanza na wewe'.

Amesema malengo ya kampeni hiyo ni pamoja na kuwahamsisha wateja wa malipo ya baada kulipa madeni yao hiyari kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa.

"Tunawahamasisha wateja wa malipo ya baada kulipa madeni yao kwa hiyari kabla ya kuchukua hatua za kisheria lakini pia tunatoa motisha kwa ulipaji kwa wakati ikiwemo msamaha wa riba kwa wateja watakaolipa madeni yao kikamilifu",Amesema.

Aidha ameongeza kuwa zoezi hilo litaenda sambamba na kuhamasisha  ulinzi wa miundombinu ya umeme ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha na kuimarisha uendelevu wa upatikanaji wa huduma bora ya umeme kwa wananchi.

Amesema zoezi hilo litahusisha pia ukaguzi wa mita za luku lengo likiwa kuhakisha luku zinafanya  kazi vizuri na hazijachezewa na wateja wasio waaminifu.

"Tunatoa elimu kwa wananchi jinsi ya kulinda miundombinu ya shirika kwani hii miundombinu ndio inayowezesha upatikanaji endelevuwa huduma ya umeme kwa ufanisi kwa kuzingatia kwamba ulinzi wa miundombinu ya umma ni wajibu wa kila mwananchi ",amesema.

Hivyo TANESCO inatoa rai kwa wateja na wananchi wote wanaodaiwa kutoa ushirikiano kwa kulipa madeni yao kwa wakati lakini pia kutoa taarifa kuhusu vitendo vya wizi wa umeme au uharibifu na wizi wa miundombinu ya umeme  kwa kushirikiana na vyombo vya dola ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kwa ukosefu wa huduma ya umeme pamoja na kuzuia hasara kwa shirika.

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.

BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali

BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali