MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani amesema Serikali imeendelea kupeleka maendeleo katika Wilaya ya Meatu ikiwemo ukamilishaji wa usambazaji umeme katika Vijiji vyote 109 vya Wilaya hiyo.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
18 Jun 2025
MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

*Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini*

*Ataka umeme utumike kuongeza thamani ya mazao, kilimo na ufugaji*.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani amesema Serikali imeendelea kupeleka maendeleo katika Wilaya ya Meatu ikiwemo ukamilishaji wa usambazaji  umeme katika Vijiji vyote 109 vya Wilaya hiyo.

Dkt. Samia ameyasema hayo Juni 17, 2025 Wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu akiwa kwenye ziara ya kikazi.

"Kama tulivyoahidi, hatujaishia hapo, kazi ya usambazaji umeme sasa inaendelea kwenye vitongoji lakini pamoja na jitihada hizi zote ninafahamu kuna changamoto ya umeme kutokuwa na nguvu ambayo inatatuliwa." Amesema Dkt. Samia

Ameeleza kuwa, Wizara ya Nishati inatatua   changamoto hiyo  ya umeme kutokuwa na nguvu  kwa kujenga  njia ya kusafirisha umeme kutoka Shinyanga hadi Simiyu na ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme.

Amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutapelekea uwepo wa umeme wenye nguvu na wa kutosha kwa ajili ya shughuli mbalimbali za uzalishaji ikiwemo Viwanda.

Amesisitiza kuwa, lengo la Serikali ni kuona wananchi wanatumia nishati ya umeme kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kuongeza thamani ya mazao, kilimo na ufugaji.

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.

BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali

BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali

HISTORIA YAANDIKWA RAIS DK.SAMIA APOKEA SH.TRILIONI 1 KAMA GAWIO NA MICHANGO MINGINE.

HISTORIA YAANDIKWA RAIS DK.SAMIA APOKEA SH.TRILIONI 1 KAMA GAWIO NA MICHANGO MINGINE.