

Kifo cha mwigizaji mashuhuri aliyeuawa katika mapigano makali kaskazini mwa Khartoum, kimewashtua wakazi wa mji mkuu wa Sudan huku ikiaminika kuwa kuna watu wengi zaidi wamenaswa katika mapigano hayo.
Kifo cha mwigizaji mashuhuri aliyeuawa katika mapigano makali kaskazini mwa Khartoum, kimewashtua wakazi wa mji mkuu wa Sudan huku ikiaminika kuwa kuna watu wengi zaidi wamenaswa katika mapigano hayo.
Asia Abdelmajid, ambaye alitimiza umri wa miaka 80 mwaka jana, alikuwa maarufu kwa uigizaji wake wa maigizo, umaarufu wake ulijulikana zaidi kutokana na utengenezaji wa tamthilia ya Pamseeka ya 1965 ambayo imehifadhiwa na huoneshwa katika Ukumbi wa michezo wa kitaifa huko Omdurman ikiwa ni kuadhimisha kumbukumbu ya mapinduzi ya kwanza ya Sudan dhidi ya kiongozi wa mapinduzi.
Anaheshimika zaidi kama mwanzilishi wa hatua hiyo na mwigizaji wa kwanza kufanya sanaa kwaajili ya kulipwa nchini, ambaye baadae alistaafu na kuwa mwalimu. Familia yake imesema alizikwa saa chache baada ya kupigwa risasi Jumatano asubuhi katika uwanja wa shule ya chekechea ambako alikuwa akifanya kazi hadi anafikwa na umauti.
Mpaka sasa haijabainika ni nani aliyefyatua risasi iliyomuua katika mapigano katika kitongoji cha kaskazini mwa Bahri, Lakini wapiganaji wa kijeshi wa Rapid Support Forces (RSF), ambao wamezuiliwa katika kambi zao, wanaendelea kupambana na jeshi la Sudan, ambalo limekuwa likishambulia zaidi vikosi vya RSF kwa njia ya anga. RSF limeeleza kuwa jeshi la serikali limekuwa likijaribu kutuma wanajeshi wa kikosi maalum cha polisi Jumatano lakini kundi hilo linadai kuwa lilizua mashambulizi yao ya ardhini.
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa pande zenye mgogoro kusitisha mapigano mara moja, kabla ya mgogoro huo kuzidi kuwa vita vya pande zote.
Makundi hasimu yanayopigana nchini Sudan yamekubali mapatano mapya ya siku saba kuanzia Alhamisi, lakini ikizingatiwa kwamba kwa sasa yanalenga kuangalia usitishaji mapigano wa kibinadamu na yale yaliyotangulia yamevunjika.
Wakazi wa Khartoum wanahisi wametelekezwa na kwamba jumuiya ya kimataifa inaonekana haiwezi kuwasuluhisha majenerali hao, kutokana na kwamba Jamii hiyo ya kimataifa ilifanikiwa kumaliza mgogoro wa wawili hao kwa kuwapatanisha baada ya kufanikisha mgawanyo wa madaraka kati yao na raia mwaka 2019 baada ya kiongozi wa muda mrefu Omar al- Bashir kupinduliwa.
MHANDISI SANGA AONGEZA MWEZI MMOJA KLINIKI YA ARDHI KIVULE KUONGEZA KASI YA UTOAJI HATI
WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.
TUKITUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA TUTAOKOA HEKTA 400,000 ZA MISITU ZINAZOTEKETEA KWA MWAKA-MJIOLOJIA NSAJIGWA.
MHANDISI SANGA AONGEZA MWEZI MMOJA KLINIKI YA ARDHI KIVULE KUONGEZA KASI YA UTOAJI HATI
SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA FURSA, KWA WAKULIMA WA MWANI TANGA
CUF KUPITISHA WAGOMBEA URAIS AGOSTI 9 MAJINA YATAJWA.
NGO's zatakiwa Kuwa Mawakala wa mabadiliko chanya katika Jamii.
Serikali Inaendelea Kuimarisha Mazingira Kuwawezesha Vijana Kuanzisha Shughuli Za Uzalishaji Mali.
DKT.SAMIA,DKT.NCHIMBI KUCHUKUA FOMU YA URAIS KESHO AGOSTI 9,2025.
TANESCO YAANZA ZOEZI LA UKAGUZI WA MITA KUBAINI UPOTEVU NA WIZI WA UMEME UNAOFANYWA NA BAADHI YA WATEJA.