

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na mgombea mwenza wake Dkt.Emmanuel Nchimbi watachukua fomu za kugombea nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.
Zoezi hilo litafanyika kesho, Agosti 9, 2025, katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla amesema kuwa hatua hiyo inaashiria kuanza rasmi kwa msimu wa kampeni za uchaguzi kwa vyama vyote vya siasa nchini.
"Baada ya kuchukua fomu, Mheshimiwa Rais atarejea Makao Makuu ya CCM hapa Dodoma, ambapo atapokelewa rasmi na viongozi pamoja na wanachama wa chama chetu, na kupata fursa ya kuwasalimia wananchi," amesema CPA Makalla.
Ameongeza kuwa, Dkt. Samia anagombea kwa awamu ya pili ya uongozi wake kwa mujibu wa Katiba, baada ya kumaliza kipindi cha kwanza cha miaka mitano, ambacho kitaisha rasmi mwaka huu.
Uchaguzi Mkuu wa Tanzania unatarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, ambapo vyama mbalimbali vya siasa vitashiriki kikatiba kuwani nafasi za Urais, Ubunge na Udiwani.
TUME YATANGAZA RATIBA YA VYAMA KUCHUKUA FOMU ZA WAGOMBEA WA URAIS
TANESCO YAANZA ZOEZI LA UKAGUZI WA MITA KUBAINI UPOTEVU NA WIZI WA UMEME UNAOFANYWA NA BAADHI YA WATEJA.
CUF KUPITISHA WAGOMBEA URAIS AGOSTI 9 MAJINA YATAJWA.
PBPA YAELEZEA MAFANIKIO YAKE YA MIAKA MINNE KATIKA UONGOZI WA RAIS DK.SAMIA.
MD TWANGE AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA UPANUZI WA VITUO VYA KUPOZA UMEME JIJINI DAR ES SALAAM.
TADB Yawawezesha Wakulima Wadogo Mikopo Yenye Dhamana Nafuu.
MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.
VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI.
Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.
SENYAMULE AIPONGEZA DIB UTOAJI WA ELIMU KWENYE MAONESHO NANENANE.