DKT.SAMIA,DKT.NCHIMBI KUCHUKUA FOMU YA URAIS KESHO AGOSTI 9,2025. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

DKT.SAMIA,DKT.NCHIMBI KUCHUKUA FOMU YA URAIS KESHO AGOSTI 9,2025.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na mgombea mwenza wake Dkt.Emmanuel Nchimbi watachukua fomu za kugombea nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
08 Aug 2025
DKT.SAMIA,DKT.NCHIMBI KUCHUKUA FOMU YA URAIS KESHO AGOSTI 9,2025.

Zoezi hilo litafanyika kesho, Agosti 9, 2025, katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla amesema kuwa hatua hiyo inaashiria kuanza rasmi kwa msimu wa kampeni za uchaguzi kwa vyama vyote vya siasa nchini.

"Baada ya kuchukua fomu, Mheshimiwa Rais atarejea Makao Makuu ya CCM hapa Dodoma, ambapo atapokelewa rasmi na viongozi pamoja na wanachama wa chama chetu, na kupata fursa ya kuwasalimia wananchi," amesema CPA Makalla.

Ameongeza kuwa, Dkt. Samia anagombea kwa awamu ya pili ya uongozi wake kwa mujibu wa Katiba, baada ya kumaliza kipindi cha kwanza cha miaka mitano, ambacho kitaisha rasmi mwaka huu.

Uchaguzi Mkuu wa Tanzania unatarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, ambapo vyama mbalimbali vya siasa vitashiriki kikatiba kuwani nafasi za Urais, Ubunge na Udiwani.

TUME YATANGAZA RATIBA YA VYAMA KUCHUKUA FOMU ZA WAGOMBEA WA URAIS

TUME YATANGAZA RATIBA YA VYAMA KUCHUKUA FOMU ZA WAGOMBEA WA URAIS

CUF KUPITISHA WAGOMBEA URAIS AGOSTI 9 MAJINA YATAJWA.

CUF KUPITISHA WAGOMBEA URAIS AGOSTI 9 MAJINA YATAJWA.

ACT WAJIPANGA KUIONDOA CCM MADARAKANI UCHAGUZI MKUU 2025.

ACT WAJIPANGA KUIONDOA CCM MADARAKANI UCHAGUZI MKUU 2025.

Chama cha National League for Democracy (NLD) Klmezinduwa  Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya  kwa Mwaka 2025

Chama cha National League for Democracy (NLD) Klmezinduwa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya kwa Mwaka 2025

KIBAHA YAANZA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

KIBAHA YAANZA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025