VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI.

Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ubungo imewataka viongozi wa dini na washirika wao kutafuta suluhu ya migogoro inayojitokeza ndani au nje ya Makanisa au Misikiti ili kudumisha misingi ya amani na umoja katika taasisi zao za dini.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
05 Aug 2025
VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI.

Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ubungo imewataka viongozi wa dini na washirika wao kutafuta suluhu ya migogoro inayojitokeza ndani au nje ya Makanisa au Misikiti ili kudumisha misingi ya amani na umoja katika taasisi zao za dini.

Akizungumza na viongozi wa dini wa Kanisa la wasabato Kwembe na Magomeni katika kikao chao cha kutafuta suluhu ya mgogoro wa ardhi wa kanisa la Waadventist Kwembe Kibamba jijini Dar es salam Katibu Tawala wa wilaya Ubungo(DAS) Hassan Mkwawa amesema kuwa viongozi wa dini ni mfano bora kwa upande wa serikali na raia wanaowazunguka hivyo wana wajibu wa kudumisha umoja na utulivu na kusisitiza kuwa endapo itatokea changamoto basi wana wajibu wa kumaliza changamoto zao pasipo kuzitoa hadharani.

"Ninawataka viongozi wa kanisa hili kuzingatia misingi ya mafundisho ya imani zao Ili kuimarisha na kudumisha amani pasipo kuweka taharuki ya changamoto zao kwani jamii inazimini Taasis za hizi kama majibu maswali yao",alisema Ndugu Mkwawa.

Katika hatua nyingine aliyekuwa Mjumbe wa Selikali ya kijiji cha Kwembe 1992 na Muumuini wa kanisa  hilo la Waadventist(Wasabato) Bw.Joshua Hamathe akithibitisha kuwa Serikali ya kijiji cha Kwembe ilitoa maeneo ya kuabudia kwa kila dhehebu wakiwemo na wao na wakaendelea na Ibada zao lakini kinachomshangaza ni jinsi viongozi wa Kanisa la Magomeni walivyowazunguka kuhusu eneo hilo la ibada walilokabidhiwa.

Hamathe akaongeza kuwa, "Nina historia nzuri juu ya eneo hili hivyo wito wangu kwa Kanisa ni kwamba tunalichafua kanisa kwa sababu nilitegemea sisi ni watu wa kiroho kwamba utatuzi wake ungekuwa rahisi zaidi na wangelirudisha eneo tulilopewa,pia ninaiomba serikali ifanye utatuzi kuhusu changamoto hii".

Kwa upande viongozi wa Magomeni Mch.Emmanuel Andrew na Mwenyekiti wa jimbo dogo Pwani ya Mashariki amesema wanasubiri suluhisho litakalofanywa na serikali tutakapokutana tena kwenye kikao kijacho.

TANESCO YAZINDUA MFUMO WA UPOKEAJI TAARIFA KWA SIRI WATAKA WANANCHI KUUTUMIA ILI KURIPOTI VITENDO VYA UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA SHIRIKA.

TANESCO YAZINDUA MFUMO WA UPOKEAJI TAARIFA KWA SIRI WATAKA WANANCHI KUUTUMIA ILI KURIPOTI VITENDO VYA UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA SHIRIKA.

ELAF YAITAKA SERIKALI KUUNDA CHOMBO MAALUMU CHA KUSHUGHULIKIA UPOTEVU WA WATU NCHINI.

ELAF YAITAKA SERIKALI KUUNDA CHOMBO MAALUMU CHA KUSHUGHULIKIA UPOTEVU WA WATU NCHINI.

MASLAHI MAPANA YA NCHI YANAZINGATIWA UTEKELEZAJI WA MRADI WA EACOP-DKT. MATARAGIO.

MASLAHI MAPANA YA NCHI YANAZINGATIWA UTEKELEZAJI WA MRADI WA EACOP-DKT. MATARAGIO.

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WANANCHI YAINGIZA SEKTA BINAFSI KUENDESHA MRADI WA MWENDOKASI.

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WANANCHI YAINGIZA SEKTA BINAFSI KUENDESHA MRADI WA MWENDOKASI.

SALALI:Tunampongeza Rais Samia Kwa Kujumuisha Watu Wenye Ulemavu Dira 2050.

SALALI:Tunampongeza Rais Samia Kwa Kujumuisha Watu Wenye Ulemavu Dira 2050.