

Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ubungo imewataka viongozi wa dini na washirika wao kutafuta suluhu ya migogoro inayojitokeza ndani au nje ya Makanisa au Misikiti ili kudumisha misingi ya amani na umoja katika taasisi zao za dini.
Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ubungo imewataka viongozi wa dini na washirika wao kutafuta suluhu ya migogoro inayojitokeza ndani au nje ya Makanisa au Misikiti ili kudumisha misingi ya amani na umoja katika taasisi zao za dini.
Akizungumza na viongozi wa dini wa Kanisa la wasabato Kwembe na Magomeni katika kikao chao cha kutafuta suluhu ya mgogoro wa ardhi wa kanisa la Waadventist Kwembe Kibamba jijini Dar es salam Katibu Tawala wa wilaya Ubungo(DAS) Hassan Mkwawa amesema kuwa viongozi wa dini ni mfano bora kwa upande wa serikali na raia wanaowazunguka hivyo wana wajibu wa kudumisha umoja na utulivu na kusisitiza kuwa endapo itatokea changamoto basi wana wajibu wa kumaliza changamoto zao pasipo kuzitoa hadharani.
"Ninawataka viongozi wa kanisa hili kuzingatia misingi ya mafundisho ya imani zao Ili kuimarisha na kudumisha amani pasipo kuweka taharuki ya changamoto zao kwani jamii inazimini Taasis za hizi kama majibu maswali yao",alisema Ndugu Mkwawa.
Katika hatua nyingine aliyekuwa Mjumbe wa Selikali ya kijiji cha Kwembe 1992 na Muumuini wa kanisa hilo la Waadventist(Wasabato) Bw.Joshua Hamathe akithibitisha kuwa Serikali ya kijiji cha Kwembe ilitoa maeneo ya kuabudia kwa kila dhehebu wakiwemo na wao na wakaendelea na Ibada zao lakini kinachomshangaza ni jinsi viongozi wa Kanisa la Magomeni walivyowazunguka kuhusu eneo hilo la ibada walilokabidhiwa.
Hamathe akaongeza kuwa, "Nina historia nzuri juu ya eneo hili hivyo wito wangu kwa Kanisa ni kwamba tunalichafua kanisa kwa sababu nilitegemea sisi ni watu wa kiroho kwamba utatuzi wake ungekuwa rahisi zaidi na wangelirudisha eneo tulilopewa,pia ninaiomba serikali ifanye utatuzi kuhusu changamoto hii".
Kwa upande viongozi wa Magomeni Mch.Emmanuel Andrew na Mwenyekiti wa jimbo dogo Pwani ya Mashariki amesema wanasubiri suluhisho litakalofanywa na serikali tutakapokutana tena kwenye kikao kijacho.
ACT WAJIPANGA KUIONDOA CCM MADARAKANI UCHAGUZI MKUU 2025.
EQUITY BANK YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA BAJAJ KWA AJILI YA KUWASAIDIA WAKULIMA
Kilundumya Aipongeza e-GA Kwa Kuimarisha Ushirikiano na Sekta ya Kilimo Kuleta Mapinduzi Kidigitali.
WIZARA YA NISHATI ENDELEENI KUSIMAMIA UFANISI WA MIRADI YA NISHATI- DED MKALAMA.
Chama cha National League for Democracy (NLD) Klmezinduwa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya kwa Mwaka 2025
TADB Yawawezesha Wakulima Wadogo Mikopo Yenye Dhamana Nafuu.
MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.
Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.
WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME
TAASISI NA ASASI ZA ELIMU YA MPIGA KURA ZATAKIWA KUZINGATIA SHERIA.