

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yametakiwa kuwa mawakala wa mabadiliko chanya katika jamii katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kwenye jamii.
Hayo yamesemwa leo Agosti 12, 2025 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt John Jingu wakati anazungumza katika Kongamano la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali linaloendelea kwa siku ya pili katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.
Dkt. Jingu amesema Mashirika hayo yanawajibu wa kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kifikra na maendeleo katika jamii kupita utekelezaji wa miradi yao mbalimbali.
“Mashirika Yasiyo Ya Kiserikali, yamesajiliwa kisheria kwa lengo la kutoa huduma na elimu katika nyanja tofauti kwa jamii hivyo mtambue kwamba ajenda ya maendeleo endelevu katika Taifa ni pamoja na kuwa mawakala wa mabadiliko chanya katika jamii” amesema Dkt Jungu.
Aidha ameeleza kwamba Mashirika hayo yanapaswa kutekeleza miradi ya uzalishaji ambayo ni endelevu na kuondoa utegemezi kutoka kwa wafadhili, kwa sababu kwa sasa Sera za nchi za Ulaya na Marekani zimebadilika.
Ameongeza kwamba Mashirika yanapaswa kujitafakari vizuri ili kuhakikisha yanakuwa njia mbadala kuendeleza huduma na miradi kwa kutumia rasilimali zinazopatikana katika maeneo yao.
Sanjari na hayo ameongoza na Kufunga moja ya mjadala wa siku ya pili ya kongamano la mwaka la mashirika yasiyo ya Kiserikali(NGOForum 2025)akisisitiza umuhimu wa upatikanaji wa fedha na ubunifu katika kuhakikisha mashirika yasiyo ya Kiserikali yanaendelea kuwa injini ya maendeleo ya jamii.
Mjadala huo ulilenga kujadili mada ya "Upatikanaji wa ufadhili na mikakati ya uendelevu Kwa mashirika yasiyo ya Kiserikali 2020/21- 2024/25 ukichambua mwenendo wa ufadhili nchini Tanzania, changamoto za kupungua kwa misaada kutoka kwa wafadhili wakubwa na mikakati bunifu ya kujitegemea.
Washiriki pia walijadili utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa uendelevu wa mashirika yasiyo ya Kiserikali (MKIUMA)2022/23- 2026/27 unaohimiza maandalizi ya mipango thabiti ya uendelevu na kuanzishwa kwa Mfuko wa Ruzuku kusaidia NGOs kupata rasilimali fedha.
WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.
TUKITUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA TUTAOKOA HEKTA 400,000 ZA MISITU ZINAZOTEKETEA KWA MWAKA-MJIOLOJIA NSAJIGWA.
MHANDISI SANGA AONGEZA MWEZI MMOJA KLINIKI YA ARDHI KIVULE KUONGEZA KASI YA UTOAJI HATI
SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA FURSA, KWA WAKULIMA WA MWANI TANGA
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAUDHUKUMU YAO HASA KATIKA KIPINDI HIKI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Serikali Inaendelea Kuimarisha Mazingira Kuwawezesha Vijana Kuanzisha Shughuli Za Uzalishaji Mali.
INEC YAMKABIDHI FOMU ZA UTEUZI MGOMBEA URAIS WA CHAMA CHA NLD DOYO HASSAN DOYO
MGOMBEA KITI CHA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA NRA ACHUKUA FOMU TUME
KADEGE WA CHAMA CHA UPDP ACHUKUA FOMU ZA URAIS
TUME YA TEHAMA NA TAASISI YA KASI KUJA MWAROBAINI WA UDUKUZI MTANDAONI.