

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya tehama nchini Dr.Nkundwe Mwasaga amesema serikali wamedhamiria kuongeza wataalamu wa teknolojia ambao watasaidia kuunda mifumo ya kutatua matatizo ya udukuzi na hatari za kimitandao.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya tehama nchini Dr.Nkundwe Mwasaga amesema serikali wamedhamiria kuongeza wataalamu wa teknolojia ambao watasaidia kuunda mifumo ya kutatua matatizo ya udukuzi na hatari za kimitandao.
Hayo ameyasema 11 Agosti 2025,jijini Dar es salam wakati akifungua mafunzo ya usalama mitandaoni yaliyoandaliwa na ofisi ya TEHAMA kwa kushirikiana na Taasisi inayoshughulika mambo ya usalama wa mitandao ya Korea kusini (KISA) yenye lengo la kujenga ufasini wa wataalamu nchini ili kuendelea kujenga uchumi wa kidigital.
Dr.Mwasaga amesema kuwa mafunzo hayo yatakayofanyika kwa siku tano yana tafsiri kubwa katika ujenzi wa uchumi wa kidigitali ambao utasaidia kuongeza wawekezaji na kipato kwa wananchi wa kawaida.
Dkt.Nkundwe amesisitiza kuwa ili mtu awe na Imani ya kutumia mifumo hiyo ya akiliunde ni lazima kuwe na mifumo ya usalama wa taarifa binafsi,kulinda faragha za watu na kumlinda mlaji wa mifumo ya kidigitali .
"Kuna jambo jipya limejitokeza sasa hivi na limeanza kuonekana lina umuhimu mkubwa yaani sasa hivi kupitia mitandao watu sio tu wanaweza wakaingilia mifumo lakini pia wanaweza kumbadilisha mtu fikra zake na kufikiria jinsi wanavyotaka wao huo unaitwa Udukuzi wa fikra na baadhi ya nchi wamesema ni hatari kwa jamii kwa hiyo tumeona ni vizuri wataalamu wetu wakajifunza ujanja gani unatumika na namna gani unavyofanywa",alisema. Dokta
Dkt.Nkundwe ametoa shukrani kwa KISA kwa kukubali kufanya mafunzo hayo nchini ambayo imepata fursa ya kuhudhuriwa na wataalamu kutoka taasisi 33 ambapo watapata ujuzi na kuwasaidia watu wengine.
"Mbinu za watu wabaya mitandaoni zinabadilika kila siku hivyo kupata elimu kutoka kwa nchi nyingine itasaidia kujifunza mambo mapya na Wakorea ni wataalam na watafanya mifumo yetu iwe vizuri zaidi kwa hiyo ni njia ambayo serikali imenuia kujenga uchumi madhubuti wa kidigitali".alisema Nkundwe
Kwa upande wake mtafiti kutoka taasisi ya KISA, Minyoung Kim amesema kuna umuhimu wa kutengeneza ushirikiano wa pamoja ili kuzishinda changamoto za mifumo ya kimitandao.
"katika nchi yetu Korea Kusini tumedhamiria kuwa na wataalamu 10,000 wenye uwezo wa kulinda mambo ya mitandao ya kidigitali".Ameongeza Minyoung.
Naye,mtaalamu wa mawasiliano ya teknolojia ya habari katika kitengo cha ulinzi wa tehama Venance Mwachabike amesema mafunzo hayo yatamsaidia kuboresha kazi zake katika kitengo anachofanyia kazi na kuongeza ufanisi lakini pia kujifunza mbinu mpya za kiteknolojia.
WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.
TUKITUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA TUTAOKOA HEKTA 400,000 ZA MISITU ZINAZOTEKETEA KWA MWAKA-MJIOLOJIA NSAJIGWA.
MHANDISI SANGA AONGEZA MWEZI MMOJA KLINIKI YA ARDHI KIVULE KUONGEZA KASI YA UTOAJI HATI
SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA FURSA, KWA WAKULIMA WA MWANI TANGA
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAUDHUKUMU YAO HASA KATIKA KIPINDI HIKI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Serikali Inaendelea Kuimarisha Mazingira Kuwawezesha Vijana Kuanzisha Shughuli Za Uzalishaji Mali.
NGO's zatakiwa Kuwa Mawakala wa mabadiliko chanya katika Jamii.
INEC YAMKABIDHI FOMU ZA UTEUZI MGOMBEA URAIS WA CHAMA CHA NLD DOYO HASSAN DOYO
MGOMBEA KITI CHA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA NRA ACHUKUA FOMU TUME
KADEGE WA CHAMA CHA UPDP ACHUKUA FOMU ZA URAIS