WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.

Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya mikopo ya SELF Microfinance Santieli Yona amewataka wananchi kabla ya kukopa wafanye tathmini ya kina kuhusu matumizi ya fedha wanazozichukua kwa ajili ya shughuli zao kwani wakijipanga vema watakuwa na uhuru,kujiamini pamoja na kuweza kurejesha mikopo yao bila matatizo yeyote.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
16 Aug 2025
WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.

Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya mikopo ya SELF Microfinance Santieli Yona amewataka wananchi kabla ya kukopa wafanye tathmini ya kina kuhusu matumizi ya fedha wanazozichukua kwa ajili ya shughuli zao kwani wakijipanga vema watakuwa na uhuru,kujiamini pamoja na kuweza kurejesha mikopo yao bila matatizo  yeyote.

Akizungumza leo 15,agosti 2025 kwenye kikao na jukwaa la Wahariri na Waandishi wa Habari Kilichoandaliwa na ofisi ya msajili wa Hazina jijini Dar es salaam Santieli amebainisha kuwa kuna changamoto ya wananchi wengi kukosa elimu ya fedha na kushindwa kufanya tathmini kabla ya kukopa ambapo husababisha baadhi watu wawe na hulka ya kutojali urejeshaji wa mikopo waliyoichukua.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa suluhuhisho ya kuzishinda changamoto za fikra potofu za ukopaji ni muhimu kuweka mkazo katika kutoa elimu kwa raia ili kuimarisha huduma za fedha kwa kuwa elimu hiyo imewafikia wachache.
Aidha bi Santieli alifafanua mafanikio  ya SELF ikiwa ni kutoa mikopo kwa ajili ya nishati safi ya kupikia ili kutekeleza agenda ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan na manufaa ya mikopo hiyo  itasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia ya nchi.

 "Moja ya mafanikio tuliyoyapata ni kutengeneza ajira,sisi tunatoa mikopo kwa taasisi zinazokopesha na wajasiriamali sasa wanapopewa fedha, wanajiajiri na kutoa fursa kwa watu wengine na katika kipindi hiki tumeweza kutoa ajira zipatazo 183,000, jambo ambalo ni mafanikio makubwa kwa taifa, kwani si serikali pekee inayoweza kutoa ajira, bali kila mmoja anaweza kujiajiri na kujikimu.,” alieleza

Hata hivyo aliongeza kuwa Microfinance yao inatoa elimu ya fedha mara kwa mara kupitia majukwaa mbalimbali, ikiwemo maonesho ya Nanenane, Sabasaba, makongamano na kupitia vyombo vya habari lengo  ni kuhakikisha wananchi wengi wanafikiwa na kusaidiwa kifikra kuhusu mikopo.

"Tuna dhamira ya kufika kila mkoa na tunawaalika Watanzania waje kushiriki na sisi kwa sababu hatuwezi kwenda peke yetu ila na wao pia huwa tunafuatilia na kuona kama huduma zetu zinabadilisha maisha ya wanufaika na niwajuze kila baada ya muda tunapenda kujua walikuwa wapi  na mikopo imenufaishaje na wapo viwango gani sasa ,” alisema Santieli

Taasis hiyo ya kifedha imelenga kuongeza mtaji wa mikopo hadi Tsh billion 300 ndani ya miaka mitano ijayo na itawafikia zaidi ya wanufaika 20000 moja kwa moja pia imeweza kujenga uwezo kwa taasisi 549 kwa kutoa ushauri mbalimbali.

PPAA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE, KUTOA ELIMU KWA WAZABUNI NA UMMA

PPAA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE, KUTOA ELIMU KWA WAZABUNI NA UMMA

Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.

Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.

WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME

WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME

DK.MPANGO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITALI KUFANYA MALIPO,AIPONGEZA BoT KUZINDUA MFUMO MKUU JUMUISHI WA KIBENKI.

DK.MPANGO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITALI KUFANYA MALIPO,AIPONGEZA BoT KUZINDUA MFUMO MKUU JUMUISHI WA KIBENKI.