

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga ameongeza mwezi mmoja kwa watumishi wanaotoa huduma za ardhi kwenye Kliniki ya Ardhi inayofanyika Kata ya Kivule Ilala Dar e salaam kuanzia Agosti 18, 2025 ili kupunguza mzingo mkubwa kwa wananchi ambao hawana hati.
Mhandisi Sanga ametoa maekelezo hayo Agosti 16, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Kivule ambao wanaendelea kupata huduma kwenye Kliniki hiyo.
“Tunatamani zoezi hili limalize changamoto zenu zote, kwa sababu tukimaliza changamoto zenu hapa hamtakuja ofisini, nawaagiza wasaidizi wangu, zoezi hili liendelee kwa muda wa mwezi mzima baada ya tarehe 18 Agosti 2025 ambayo ilipangwa ili kumaliza changamoto zenu za ardhi katika maeneo yenu” amesema Mhandisi Sanga.
Ili kuleta tija katika zoezi hilo, Mhandisi Sanga ameelekeza watumishi 10 waongezwe katika kliniki hiyo ambao watatoka maeneo mbalimbali nchini ili kuongeza kasi ya utoaji hati kwa tija, wataongezewa vifaa na kuunda timu za kuwafuata wananchi kwenye maeneo yao ikiwemo mtaa wa Mbondole kata ya Kivule.
Aidha, amewaasa watumishi wa sekta ya ardhi wanaotoa huduma kwa wananchi maeneo mbalimbali nchini, wasiwavuruge wananchi watoe huduma kadiri mwananchi anavyofika kwenye eneo la huduma ili kuondoa kero na kuweka utaratibu unaofaa kuwahudumia wananchi kulingana na walivyofika na kupata huduma kama serikali inavyoelekeza.
Kwa upande wake Bw. Juma Saidi Msimbazi mkazi wa Kivule ameridhishwa na huduma inayotolewa na Wizara ya Ardhi katika eneo lao kwa kuwasogezea huduma karibu zaidi na hali ikiendelea hivyo nchi itapiga hatua kubwa katika maendeleo.
Kliniki ya Ardhi kama hiyo ya Ilala Dar es Salaam inaendeshwa pia katika mikoa ya Dodoma, Mpunguzi, Mbeya, wilaya ya Mbarali na Shinyanga katika Manispaa ya Shinyanga na Wilaya ya Kahama.
WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.
TUKITUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA TUTAOKOA HEKTA 400,000 ZA MISITU ZINAZOTEKETEA KWA MWAKA-MJIOLOJIA NSAJIGWA.
SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA FURSA, KWA WAKULIMA WA MWANI TANGA
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAUDHUKUMU YAO HASA KATIKA KIPINDI HIKI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANAWAKE MKOANI MBEYA
Serikali Inaendelea Kuimarisha Mazingira Kuwawezesha Vijana Kuanzisha Shughuli Za Uzalishaji Mali.
NGO's zatakiwa Kuwa Mawakala wa mabadiliko chanya katika Jamii.
INEC YAMKABIDHI FOMU ZA UTEUZI MGOMBEA URAIS WA CHAMA CHA NLD DOYO HASSAN DOYO
MGOMBEA KITI CHA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA NRA ACHUKUA FOMU TUME
KADEGE WA CHAMA CHA UPDP ACHUKUA FOMU ZA URAIS