PPAA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE, KUTOA ELIMU KWA WAZABUNI NA UMMA | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

PPAA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE, KUTOA ELIMU KWA WAZABUNI NA UMMA

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) inashiriki Maonesho ya NaneNane Kitaifa yanaendelea katika Viwanja vya Maonesho vya Nzuguni Jijini Dodoma kutoa elimu kuhusu ununuzi wa Umma kwa wazabuni, hususan elimu kuhusu Moduli ya kupokea na kushughulikia Malalamiko na Rufaa katika mfumo wa NeST

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
03 Aug 2025
PPAA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE, KUTOA ELIMU KWA WAZABUNI NA UMMA

Akiongea kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Bw. Nelson Kessy amesema PPAA imejipanga kutoa elimu kwa wadau wa ununuzi wa umma na wananchi kwa ujumla ili kutoa wigo mpana zaidi kwa wazabuni na wadau wa sekta hiyo.

Pamoja na mambo mengine, Bw. Kessy amewasihi wadau wa ununuzi na wananchi kwa ujumla kutembelea Banda la PPAA linalopatikana ndani ya Banda la Wizara ya Fedha katika viwanja vya Nzuguni, Dodoma.

Maonesho haya kwa mwaka 2025 yamebeba kauli mbiu “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”. Maonesho ya NaneNane Kitaifa yalifunguliwa rasmi tarehe 1 Agosti, 2025 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mapango. Maonesho hayo yalianza tarehe 1 hadi 8 Agosti 2025.

Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.

Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.

WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME

WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME

DK.MPANGO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITALI KUFANYA MALIPO,AIPONGEZA BoT KUZINDUA MFUMO MKUU JUMUISHI WA KIBENKI.

DK.MPANGO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITALI KUFANYA MALIPO,AIPONGEZA BoT KUZINDUA MFUMO MKUU JUMUISHI WA KIBENKI.