Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama ametoa agizo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe kwamba vituo vyote vinavyotoa huduma za afya hapa nchini viweke wazi mikataba ya utoaji huduma bora kwa mteja ili kuepuka migogoro na migongano baina ya watoa huduma na wateja na pia akishangazwa na vitendo vya kuzuia maiti kwa madai ya madeni vilivyojitokeza kwa vipindi tofauti tofauti.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
25 Jun 2025
Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja

Kauli hiyo ameitoa June 25 mwaka huu akizindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja katika ukumbi wa Wizara ya Afya Jijini Dodoma ambapo amesema mkataba huo ni ahadi baina ya Wizara ya Afya na Wananchi na unalenga kutoa huduma bora,sahihi na kwa wakati hivo kuleta mabadiliko makubwa katika utoaji wa huduma za afya hatua ambayo itaongeza uwajibikaji  kwa watendaji wa sekta hiyo.

"Na nyie mmeona wakati mwingine  kumekuwa na ugumu wa kutekeleza miongozo inayohusiana na huduma za hifadhi ya maiti,inabaki kuwa kelele maiti inashikiliwa eti inadaiwa,na ndio maana niliwaambia sasa maiti huyo kama alikuwa anajilipia mwenyewe matokeo yake ni nini? Tunataka afufuke ndo aende kujilipia?" Amesema Mhagama

Aidha ameagiza vituo vyote vinavyotoa huduma za afya vizingatie matumizi ya mifumo iliyowekwa kuhusiana na utoaji wa huduma za afya nchini  ili kupunguza malalamiko yasiyo ya msingi.

"Inakuwaje mgonjwa anaporuhusiwa ama kinapotokea kifo kituo cha kutolea huduma kinasema tunakudai, mgonjwa yeye anadai kwamba ameshalipa jambo gani limejificha na limejificha wapi? Tunataka watu wawe na mikataba na kila jambo liwe wazi ili tukiweza kutengeneza uwazi tutawabaini wale ambao hawana uwezo."Amesema Mhagama

Hata hivyo amesema kwamba huduma ambazo zimetajwa kwenye mkataba huo zinaendana na sera na miongozo mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za afya nchini,ushauri wa kitaalamu kuhusu uendeshaji wa shughuli za afya,maswala ya chanjo,vyeti vya usajili wa kitaaluma,leseni za kitaaluma,vibali mbalimbali,taarifa za sekta ya afya,mikataba ya kimataifa waliyoingia nayo,mikataba  ya ndani na huduma nyinginezo.

"Kupitia Mkataba huu wa huduma kwa mteja Wizara ya Afya niwahakikishie tumejipanga Vizuri kuyatekeleza hayo kwa ubora unaotakiwa." Amesema Mhagama

Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma

Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma

Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake

Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake

CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA KUWA VINARA WA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME NA KUDUMISHA AMANI KWENYE MITAA YAO.

CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA KUWA VINARA WA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME NA KUDUMISHA AMANI KWENYE MITAA YAO.

Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.

Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.

LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA

LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA