

Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi (UVCCM)wametoa onyo kwa wanaharakati na wanasiasa wasio na nia kwa taifa kuacha propaganda za upotoshaji kwani hakuna mwenye mamlaka ya kuzuia uchaguzi usifanyike hapa nchini.
Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi (UVCCM)wametoa onyo kwa wanaharakati na wanasiasa wasio na nia kwa taifa kuacha propaganda za upotoshaji kwani hakuna mwenye mamlaka ya kuzuia uchaguzi usifanyike hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya vijana CCM iliyopo Upanga jijini Dar es salaam mwanachama kijana Magula Marko Magula amesema kwamba hakuna mwananchi wala chama chochote chenye mamlaka kuzuia uchaguzi kwa kuwa uchaguzi ni swala la kikatiba na haki ya kila mwananchi
Aidha Magula ameongeza kuwa "Kila chama Cha siasa kina haki ya kushiriki au kutokushiriki uchaguzi hivyo kama kuna chama cha siasa hakijajipanga kuingia katika zoezi hili basi wasituharibie uchaguzi ".
Pia amewataka watanzania kushiriki kikamilifu katika zoezi la kupiga kura na kuwataka vijana kuchukua fomu za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi
Katika hatua nyingine kijana na mwanachama hai wa chama hicho ndugu Isaack Sumbaru amesema kuwa hakuna umma wowote utakaozuia uchaguzi kwani amani ndio tunu ya watanzania.
Aidha Isaack amesema kuwa " Niwahakikishie wananchi mabadiliko ya sheria ya uchaguzi yamefanyika kwa sababu kumekuwa na upotoshaji kwamba hakuna kilichofanyika na sote tukubaliane kwamba tume huru ya uchaguzi ipo kikatiba haijatungwa na mtu from nowhere na tume yetu ni miongoni mwa tume bora sana hapa Africa na Africa mashariki"
Pia Isaack ameongeza kuwa hapo awali tume ilikuwa hajiwezi kujiendesha yenyewe lakini hivi sasa inajiendesha kwa fedha za ndani,hivyo gharama zote zitagharamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,vilevile utenda katika tume imeboreshwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja.
Wenye malori watakiwa kuweka vifaa vya usalama
Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma
Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake
Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja
GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.
CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.
PPAA yatoa elimu matumizi ya Moduli Wiki ya Utumishi wa Umma