CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA KUWA VINARA WA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME NA KUDUMISHA AMANI KWENYE MITAA YAO. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA KUWA VINARA WA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME NA KUDUMISHA AMANI KWENYE MITAA YAO.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ndugu Albert Chalamila ametoa rai kwa wenyekiti wa serikali za mitaa na watendaji wake kutambua umuhimu wa kulilinda taifa lao kwani wao ndio wenye dhamana ya kuhakikisha wanatetea ulinzi na amani

Ngonise Kahise
By Ngonise Kahise
25 Jun 2025
CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA KUWA VINARA WA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME NA KUDUMISHA AMANI KWENYE MITAA YAO.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ndugu Albert Chalamila ametoa rai kwa  wenyekiti wa serikali za mitaa  na watendaji wake kutambua umuhimu wa kulilinda taifa lao kwani wao ndio wenye dhamana ya kuhakikisha wanatetea ulinzi na amani.

 Rai hiyo aliitoa Leo June 24 2025 katika kikao cha shirika la umeme TANESCO na wenyekiti wa serikali za mitaa halmashauri ya Kinondoni na Ubungo pamoja na watendaji mbali mbali katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam

"Mara nyingi watendaji wa serikali wanazungumzia madili na faida wanazozipata kwenye uongozi bila kujali usalama wa mitaa yao lakini kama ninyi hamtakua wasimamizi wazuri katika mitaa yenu mshahara wa uzembe unaweza kuwadondokea ninyi wenyewe viongozi wa serikali za mitaa" alisema Chalamila

Aidha kiongozi huyo ameeleza kuwa shirika la umeme TANESCO limefanya kazi kubwa katika kuzuia wizi wa mafuta pamoja na ushushaji wa transifoma hivyo amewataka watendaji hao kusimamia ulinzi wa miundombinu ya umeme katika mitaa yao .

Katika hatua nyingine mkurugenzi wa TANESCO Bw.Lazaro Twagi amezungumza kuwa swala la utekelezaji wa miradi ya umeme uko kwenye mkono wa serikali za mitaa kwa sababu wananchi ndio wateja wakuu wa umeme hivyo amedhamiria kutengeneza mfumo mzuri wa mawasiliano ili kuboresha huduma zao.

Mkurugenzi ametoa wito kwa viongozi hao kuwa daraja kati yao na wananchi hususan pale wananchi wanapohitaji kupata taarifa juu ya miradi ya shirika hilo

Katika kutengeneza urafiki wa kistratejia shirika la umeme limeweka dhamira ya dhati ya kuwafikia wenyeviti wote nchini ili kusikia sauti za wananchi juu ya huduma zao

Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma

Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma

Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake

Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake

Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja

Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja

Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.

Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.

LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA

LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA