Machali Apongeza Ubunifu wa Vijana UDSM,Awataka Wafugaji wa Samaki Kujifunza Teknolojia Mpya Zinazoboresha Sekta Hiyo | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kilimo

Machali Apongeza Ubunifu wa Vijana UDSM,Awataka Wafugaji wa Samaki Kujifunza Teknolojia Mpya Zinazoboresha Sekta Hiyo

MWENYEKITI wa Kamati ya Itifaki ya Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) Kitaifa mwaka 2025, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali, amewataka wafugaji wa samaki nchini kujitokeza kwa wingi kutembelea mabanda ya taasisi za elimu ili kujifunza teknolojia mpya zinazoboresha sekta hiyo.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
07 Aug 2025
Machali Apongeza Ubunifu wa Vijana UDSM,Awataka Wafugaji wa Samaki Kujifunza Teknolojia Mpya Zinazoboresha Sekta Hiyo

Akizungumza baada ya kutembelea mabanda mbalimbali kwenye maonesho hayo yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma, Machali alisema amevutiwa na ubunifu wa mabinti wanaojihusisha na utengenezaji wa mafuta asilia yanayosaidia kuondoa mikunjo ya ngozi.

Machali pia alieleza kufurahishwa na teknolojia mpya inayotumika katika ufugaji wa samaki, ikiwemo mashine maalum zinazotumika kukamata vifaranga vya samaki bila kutumia mikono, hatua ambayo husaidia kupunguza vifo vya samaki wachanga ambavyo kwa kawaida hujitokeza endapo wanashikwa kwa mikono.

Amesisitiza kuwa matumizi ya teknolojia hizo ni muhimu kwa wafugaji wote wa samaki ili kuboresha uzalishaji na kuokoa mifugo midogo isiyokomaa.

Katika hatua nyingine, Machali amelitaja Banda la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Ndaki ya Masuala ya Kilimo na Teknolojia, kuwa ni eneo muhimu kwa wakulima na wafugaji kutembelea na kujifunza teknolojia mbalimbali zinazohusiana na kilimo cha kisasa.

Ameeleza kuwa moja ya teknolojia za kuvutia zinazopatikana katika banda hilo ni mtandao wa kidijitali unaowaunganisha wakulima moja kwa moja na maafisa ugani, kwa njia inayofanana na mfumo wa kuomba usafiri kwa kutumia simu za mkononi.

Maonesho ya Nanenane mwaka 2025 yameendelea kuvutia washiriki kutoka sekta mbalimbali, yakiongozwa na kaulimbiu isemayo: “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.”

EQUITY BANK YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA BAJAJ KWA AJILI YA KUWASAIDIA WAKULIMA

EQUITY BANK YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA BAJAJ KWA AJILI YA KUWASAIDIA WAKULIMA

Kilundumya Aipongeza e-GA Kwa Kuimarisha Ushirikiano na Sekta ya Kilimo Kuleta Mapinduzi Kidigitali.

Kilundumya Aipongeza e-GA Kwa Kuimarisha Ushirikiano na Sekta ya Kilimo Kuleta Mapinduzi Kidigitali.

Coop Benki na AGITIF Watenga Shilingi Bilioni 8.5 kwa Mikopo ya Wakulima Vijana na Vyama vya Ushirika.

Coop Benki na AGITIF Watenga Shilingi Bilioni 8.5 kwa Mikopo ya Wakulima Vijana na Vyama vya Ushirika.

TADB Yawawezesha Wakulima Wadogo Mikopo Yenye Dhamana Nafuu.

TADB Yawawezesha Wakulima Wadogo Mikopo Yenye Dhamana Nafuu.

SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.

SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.