Wizara ya Afya Imesisitiza Umuhimu wa Elimu ya Afya ya Uzazi Kwa Watoto na Vijana. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

Wizara ya Afya Imesisitiza Umuhimu wa Elimu ya Afya ya Uzazi Kwa Watoto na Vijana.

Wizara ya Afya imesisitiza umuhimu wa elimu ya afya ya uzazi kwa watoto na vijana, pamoja na upatikanaji wa chanjo ya HPV kwa wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 14, kama hatua ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa hatari wa Saratani ya Mlango wa Kizazi.

Moreen Rojas  Dodoma.
By Moreen Rojas Dodoma.
25 Apr 2025
Wizara ya Afya Imesisitiza Umuhimu wa Elimu ya Afya ya Uzazi Kwa Watoto na Vijana.

Pia, wanawake  wamehimizwa kufanya uchunguzi wa mara kwa mara ili kugundua ugonjwa huo mapema na kupata matibabu stahiki.

Hayo yameelezwa na Kaimu Meneja mpango wa taifa wa chanjo Lodalis Gadao Aprili 24, 2025 Jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari katika madhimisho ya wiki ya chanjo kitaifa.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Gadao amesema, tatizo hili ambalo huwakumba wanawake hutokea kwenye mlango wa kizazi katika sehemu inayounganisha mfuko wa uzazi (Uteras) Pamoja na uke (Vagina) kutokana na seli za mlango huu  kukua kwa kasi isiyo ya kawaida.

Aidha amesema Licha ya jitihada zinazofanywa na serikali kupitia Wizara ya Afya, na wadau mbalimbali  kukabiliana na ugonjwa wa saratani ya malango wa kizazi  bado tatizo hili  limendelea kuwa tishio.

Tatizo la ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi limezidi kuwa tishio licha ya jitihada zinazofanywa na serikali kupitia Wizara ya Afya na wadau mbalimbali kukabiliana na changamoto hiyo.

Hata hivyo takwimu zilizotolewa na taasisi ya Saratani ya Ocean Road imeonyesha kuwa  takribani asilimia 36 ya vifo vinavyotokana na ugonjwa Saratani nchini husababishwa na aina hii ya saratani.

Lakini pia wizara ya afya imesema zaidi ya wanawake 10,000 huambukizwa saratani ya mlango wa  kizazi kila mwaka, huku  zaidi ya wanawake 6,000 wakipoteza Maisha kutokana na ugonjwa huu.

Kaimu Meneja mpango wa taifa wa chanjo Lodalis Gadao amesema, ugonjwa huo kwa sasa ni tishio kwa  wanawake, kutokana na  uelewa mdogo juu ya ugonjwa huo Pamoja na mwitikio mdogo  kwa wanawake kujitokeza kupata chanjo.

“Wanawake wengi hawana utamaduni wa Kwenda vituoni kupima afya zao hivyo inapelekea ugumu  kugundua mapema kama wana tatizo hili ili  kuanza matibabu mapema jambo linaloleta ufanisi katika uponaji.”Amesema Gadao.

Amesema wanawake wengi  hufika hospitali wakiwa tayari wako katika hatua za mwisho za ugonjwa huu hivyo kupata matibabu ambayo huweza kupelekea kupona au  kupoteza Maisha.

“Asilimia zaidi ya 70 ya wagonjwa wanaofika hospitali kupata matibabu, hufika kwa kuchelewa sana, na wanakuja wakiwa katika hatua ya mwisho jambo linalopelekea ugumu katika uponaji wa tatizo hili.”Amesema.

Hata hivyo amewataja wanawake walio na maambukizi ya VVU kuwa kundi hatari zaidi kuambukizwa ugonjwa huu, kutokana kudhurika kwa maumbile yao ambayo huwezesha kirusi hiki kukaa kwa urahisi.

Aidha katika  taarifa hiyo pia Gadau  amebainisha kuwa watoto wa kike wanaoanza kujihusisha na ngono katika umri mdogo wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa aina hii ya  saratani.

Amesema uchunguzi wa hivi karibuni umeonyesha kuwa kati ya Watoto wakike wanne wanaojihusisha na mapenzi katika umri mdogo watatu hupata maambukizi ya  ugonjwa huu.

Mbali na hatari za ugonjwa huu Gadao pia ametaja mikakati mbalimbali inayoendelea  ili kutokomeza tataizo hili, ikiwemo utoji wa chanjo kwa Watoto wadogo   wenye umri kuanzia miaka 9.

Lakini pia kuwakinga watoto wa kike wenye umri mdogo, kushiriki katika mahusiano ya kimapenzi.

Lakini pia ameitaka jamii kubadilika, na kuachana mara moja na tabia ya kushiriki kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja.

’’Kitu kingine ambacho kitasaidia kuepukana na ugonjwa huu kwa wanawake ni kubadili tabia yakuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwananume Zaidi ya mmoja, kwasababu kirusi hiki huambukizwa kwa njia ya kujamiiana na hupatikana kwa wanaume.’’Amesema.

Kwa upande wake Afisa Programu wa Elimu ya kwa umma katika mpango wa taifa wa chanjo Dk.Tumaini Haonga amesema licha ya kuwepo kwa utaratibu wa utoaji wa chanjo ya ugonjwa huu bado zipo baadhi ya changamoto ambazo husababisha walengwa kutokupata chanjo au kushindwa kumaliza dozi.

Amesema baadhi ya wanajamii hususani wafugaji na wakulima hushindwa kufikiwa kwa urahisi wakati wa utoaji wa chanjo  kutokana na tabia kuhamahama ili kuendesha shughuli zao.

Lakini pia baadhi ya wazazi wanaoishi mijini kushindwa kuwafikisha Watoto wao kupata huduma ya chanjo kutokana na kukosa muda.

’’Changamoto tunazokutana nazo ni baadhi ya wazazi wanaoishi mijini hushindwa kuwapeleka watoto wao kupata huduma ya chanjo kutokan kubanwa na kazi jambo linalorudisha nyuma mapambano dhidi ya ugonjwa huu.’’Amesema Haonga.

JWTZ YATANGAZA Nafasi Kwa Vijana wa Kitanzania.

JWTZ YATANGAZA Nafasi Kwa Vijana wa Kitanzania.

Kiwango Cha Maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria Kimepungua Kwa takribani asilimia 45

Kiwango Cha Maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria Kimepungua Kwa takribani asilimia 45

Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa kazi Kufanyika Singida.

Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa kazi Kufanyika Singida.

Waziri Simbachawene "Sio Lazima Kila Mhitimu Aajiriwe na Serikali"

Waziri Simbachawene "Sio Lazima Kila Mhitimu Aajiriwe na Serikali"

TASAC YAWAJENGEA UWEZO MAWAKALA WA MELI, FORODHA NA WAKUSANYAJI NA WATAWANYAJI WA MIZIGO MWANZA.

TASAC YAWAJENGEA UWEZO MAWAKALA WA MELI, FORODHA NA WAKUSANYAJI NA WATAWANYAJI WA MIZIGO MWANZA.