BODI YA TASAC:SERIKALI IMEWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA BANDARI ZOTE NCHINI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

BODI YA TASAC:SERIKALI IMEWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA BANDARI ZOTE NCHINI.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Uwakala Meli Tanzania (TASAC), Nahodha Mussa Mandia amesema kuwa Serikali imeweka mikakati ya kuimarisha bandari zote nchini pamoja mialo ya Uvuvi ili kuongeza huduma za maendeleo kwa wananchi.

NICHOLAUS KINYARIRI (OUT).
By NICHOLAUS KINYARIRI (OUT).
28 Apr 2025
BODI YA TASAC:SERIKALI IMEWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA BANDARI ZOTE NCHINI.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Uwakala Meli Tanzania (TASAC), Nahodha Mussa Mandia amesema kuwa Serikali imeweka  mikakati ya kuimarisha bandari zote nchini pamoja mialo ya Uvuvi ili kuongeza  huduma za maendeleo kwa wananchi.

Nah.Mandia ameyasema hayo wakati Bodi hiyo ilipotembelea Bandari ya Magarini na Mwalo wa Lwazi katika Wilaya Muleba mkoani Kagera.

Amesema kuwa kama wadhibiti kazi yao kuangalia usalama wa Bandari, Mialo ya Uvuvi pamoja na shughuli zinazofanyika katika maeneo hayo katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na salama ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa Taifa.

“Miradi inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali inatokana na rasilimali zilizopo kwa sasa na maeneo  ambayo bado serikali inaendelea kufanyia kazi na kuwataka wananchi kuwa na subira huku wakiendelea kufanya shughuli zao"Amesema.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kikuku Abdul Hassan amesema changamoto yao katika Mwalo wa Lwazi ni kukosekana kwa Ghati ya kuegeshea vyombo vya usafiri maji hivyo ameiomba ³Serikali kutatua changamoto hiyo ambapo itasaidia kuongeza vyombo vya usafiri wa majini vinavyohudumia wananchi wa visiwa mbalimbali.

Amesema kuwa ziara ya Bodi ya TASAC ni moja ya njia ya Serikali kuwafikia wananchi kuwasikiliza na kushauriana ili kupata mwanga katika utatuzi wa changamoto zao.  Amewaomba wananchi waendelee kuwa na imani ya Rais Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kazi yake katika kutatua changamoto kwa wananchi wake na kuwaletea maendeleo.

Nae,Mwenyekiti wa Umoja wa Wasafirishaji wa Bandari ya Magarini amesema kuwa wanaishukuru TASAC kwa kuwapa elimu ya usalama wa vyombo vya majini ambapo wanaendelea kuwa kujisimamia kutokana na elimu hiyo.

WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI.

WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI.

Wananchi wa mialo na ziwa waiomba serikali kuboresha miundombinu

Wananchi wa mialo na ziwa waiomba serikali kuboresha miundombinu

BODI YA WAKURUGENZI  TASAC YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI ZA KEMONDO NA BUKOBA.

BODI YA WAKURUGENZI TASAC YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI ZA KEMONDO NA BUKOBA.

TPDC,  ZPDC  ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI.

TPDC, ZPDC ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI.

TIB IMEWEKEZA SHILINGI BILIONI 630.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO.

TIB IMEWEKEZA SHILINGI BILIONI 630.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO.