BODI YA WAKURUGENZI TASAC YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI ZA KEMONDO NA BUKOBA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

BODI YA WAKURUGENZI TASAC YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI ZA KEMONDO NA BUKOBA.

Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imesema kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika miradi ya ujenzi wa Bandari za Kemondo na Bukoba hivyo fedha hizo zinatakiwa kuleta tija na zirudi kutokana huduma zitazotolewa na Bandari hizo.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
26 Apr 2025
BODI YA WAKURUGENZI  TASAC YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI ZA KEMONDO NA BUKOBA.

Bodi ya Wakurugenzi  wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imesema kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika miradi ya ujenzi wa Bandari za Kemondo na Bukoba hivyo fedha hizo zinatakiwa kuleta tija na zirudi kutokana huduma zitazotolewa na Bandari hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati ziara Bodi katika Bandari hizo Mwenyekiti wa Bodi hiyo Nah.Mussa Mandia amesema kuwa baada ya maboresho ya miundombinu ya ujenzi wa bandari watahudumia mizigo na abiria kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na ilivyokuwa awali.

"Fedha ya Bandari ya Kemondo bilioni 20 na ujenzi wake umekamilika ambapo huduma zake zimeongezeka hadi kufikia tani 150000 kwa mwezi na mapato yake yameongezeka mara tatu huku Bandari ya Bukoba ujenzi wake ukiwa katika hatua za mwisho na  unaogharimu zaidi ya sh.Bilioni 19",Amesema.

Amesema  kuwa kama wadhibiti ni kuhakikisha Bandari hizo zinaendelea kutoa huduma bora na tija kwa serikali huku akitaka wasimamizi wa bandari kusimamia kwa  weledi.

Amesema Serikali ya awamu ya Sita chini  ya uongozi wa Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweza kutimiza ndoto katika upanuzi wa bandari za Kemondo na Bukoba ambapo miundombinu yake ilikuwa ya zamani na ilikuwa haiendani na mahitaji ya sasa.

Hata hivyo amesema bodi itaendelea kushauri katika taasisi wanayoidhibiti ambapo matokeo yake yataendelea kuonekana  kwa miradi mbalimbali kwenye bandari za nchi nzima

Mtendaji mkuu wa  Bandari ya Bukoba wa TPA Malick Ismail amesema kuwa maboresho ya ujenzi wa bandari hiyo baada ya kukamilika watahudumia meli nne kwa wakati mmoja tofauti na ilivyokuwa awali ambapo walikuwa wakihudumia meli moja.

Bodi hiyo ilitembelea Bandari ya Kemondo ,Bukoba pamoja na kiwanda cha  Vic Fish TASAC inadhibiti uzito kwa ajili ya Usafirishaji wa Samaki nje ya nchi.

WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI.

WANANCHI LUHITA WALIA NA MAGUGU ZIWA BURIGI.

Wananchi wa mialo na ziwa waiomba serikali kuboresha miundombinu

Wananchi wa mialo na ziwa waiomba serikali kuboresha miundombinu

BODI YA TASAC:SERIKALI IMEWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA BANDARI ZOTE NCHINI.

BODI YA TASAC:SERIKALI IMEWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA BANDARI ZOTE NCHINI.

TPDC,  ZPDC  ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI.

TPDC, ZPDC ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI.

TIB IMEWEKEZA SHILINGI BILIONI 630.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO.

TIB IMEWEKEZA SHILINGI BILIONI 630.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO.