DrKumbuka Afunguka Kuhusu Kuvunjika kwa Ndoa ya Haji Manara na Zaiylissa | The Dodoma Post
The Dodoma Post Burudani

DrKumbuka Afunguka Kuhusu Kuvunjika kwa Ndoa ya Haji Manara na Zaiylissa

Mtangazaji maarufu wa kituo cha redio cha EFM, #DrKumbuka, ametoa kauli kali kuhusu kuvunjika kwa ndoa ya aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba, #HajiManara, na mrembo wake #Zaiylissa.

Gilbert ludovick
By Gilbert ludovick
11 Apr 2025
DrKumbuka Afunguka Kuhusu Kuvunjika kwa Ndoa ya Haji Manara na Zaiylissa

Akizungumza kwenye kipindi chake, #DrKumbuka amesema kuwa, “Mwanaume kurogwa kwenye mapenzi ni kitu cha kawaida kabisa. Wengine tunarogwa kimapenzi na hatujui.”

Kauli hiyo imekuja baada ya taarifa kusambaa mtandaoni zikionesha kuwa ndoa ya Manara na Zaiylissa imevunjika rasmi, huku wawili hao wakidaiwa kutoleana vitu vya ndani na kuacha nyumba ikiwa tupu.

Katika ushauri wake kwa Haji Manara, Dr Kumbuka alieleza kuwa endapo atahitaji kufunga ndoa tena, ni muhimu kutafuta mwanamke aliyekomaa kiakili, kihisia, na ambaye wanalingana kiumri.

“Ndoa si picha za Instagram, ni maisha halisi. Tafuta mtu ambaye amemaliza kila kitu – siyo bado yupo kwenye kipindi cha kujaribu maisha.” – aliongeza.

Hadi sasa, Manara hajatoa kauli rasmi kuhusu kilichojiri, lakini mashabiki wake mitandaoni wameendelea kumshauri apumzike kwanza kabla ya kurudi tena kwenye anga za mapenzi.

Serikali imeratibu jumla ya matamasha matatu ya Kitaifa ya utamaduni.

Serikali imeratibu jumla ya matamasha matatu ya Kitaifa ya utamaduni.

WASANII WAPEWA MAFUNZO YA KUGEUZA SANAA KUTOKA KUWA BURUDANI HADI BIASHARA.

WASANII WAPEWA MAFUNZO YA KUGEUZA SANAA KUTOKA KUWA BURUDANI HADI BIASHARA.

Jay Z na Familia Yake Wapata Vitisho Kufuatia Kesi ya Ubakaji

Jay Z na Familia Yake Wapata Vitisho Kufuatia Kesi ya Ubakaji

"A$AP Rocky Amzuia  rafiki yake Twelvyy Kujibu Maswali Mahakamani"

"A$AP Rocky Amzuia rafiki yake Twelvyy Kujibu Maswali Mahakamani"

KANYE WEST AMUOMBA TRUMP KUMUACHIA HURU NDUGU YAKE SEAN "DIDDY"

KANYE WEST AMUOMBA TRUMP KUMUACHIA HURU NDUGU YAKE SEAN "DIDDY"