

Mtangazaji maarufu wa kituo cha redio cha EFM, #DrKumbuka, ametoa kauli kali kuhusu kuvunjika kwa ndoa ya aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba, #HajiManara, na mrembo wake #Zaiylissa.
Akizungumza kwenye kipindi chake, #DrKumbuka amesema kuwa, “Mwanaume kurogwa kwenye mapenzi ni kitu cha kawaida kabisa. Wengine tunarogwa kimapenzi na hatujui.”
Kauli hiyo imekuja baada ya taarifa kusambaa mtandaoni zikionesha kuwa ndoa ya Manara na Zaiylissa imevunjika rasmi, huku wawili hao wakidaiwa kutoleana vitu vya ndani na kuacha nyumba ikiwa tupu.
Katika ushauri wake kwa Haji Manara, Dr Kumbuka alieleza kuwa endapo atahitaji kufunga ndoa tena, ni muhimu kutafuta mwanamke aliyekomaa kiakili, kihisia, na ambaye wanalingana kiumri.
“Ndoa si picha za Instagram, ni maisha halisi. Tafuta mtu ambaye amemaliza kila kitu – siyo bado yupo kwenye kipindi cha kujaribu maisha.” – aliongeza.
Hadi sasa, Manara hajatoa kauli rasmi kuhusu kilichojiri, lakini mashabiki wake mitandaoni wameendelea kumshauri apumzike kwanza kabla ya kurudi tena kwenye anga za mapenzi.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege