

Kesi inayomhusu rapa maarufu A$AP Rocky imeendelea kuibua maswali baada ya tukio la kipekee kutokea mahakamani. Katika kusikiliza kwa kesi ya shambulio mapema jana, A$AP Rocky alijitokeza kumzuia rafiki yake, A$AP Twelvyy, asijibu swali lililoulizwa na mahakama, jambo lililosababisha hali ya kutatanisha.
Waendesha mashtaka walimhoji Twelvyy kuhusu picha ya kitanda cha Rocky kilichoandikwa neno "AWGE", wakitaka kujua maana yake. Kabla Twelvyy hajatoa majibu, Rocky alikurupuka kwa kupaza sauti akisema, "Usiseme!" Hali hiyo ilisababisha hali ya mshikamano, huku Twelvyy akijibu kwa upole, "Inamaanisha AWGE."
Hata hivyo, mwendesha mashtaka alikasirishwa na ukimya wa Twelvyy, na aliiomba mahakama iamulie kumlazimisha kutoa majibu ya moja kwa moja. Hata hivyo, Twelvyy alikataa kusema chochote zaidi kuhusu maana ya herufi hizo nne. Wakili wa A$AP Rocky, Joe Tacopina, alijitokeza kuomba mazungumzo ya faragha na jaji ili kuzuia kuendelea kwa uchunguzi huu.
Mwisho wa siku, Twelvyy alikataa kufichua siri hiyo ya "AWGE", inayodaiwa kuwa ni shirika la ubunifu lilioanzishwa na Rocky mwaka 2014. Kwa mujibu wa taarifa, kanuni kuu ya AWGE ni ‘Kamwe usifichue maana ya AWGE’.
A$AP Rocky, ambaye anahusishwa na mashtaka mawili ya uhalifu, anadaiwa kumshambulia kwa risasi rafiki yake wa zamani na mshirika wa kundi la muziki la ASAP Mob.
NFMC kushirikiana na Nesch Mintech kuanzisha maabara ya kisasa Saudi Arabia
Dkt.Tulia Aweka Jiwe La Msingi Ujenzi wa Shule ya Wavulana Bunge.
Waziri Mhagama ametoa Agizo Vituo Vyote Vinavyotoa Huduma za Afya Viweke Wazi Mikataba Kwa Wateja.
Wenye malori watakiwa kuweka vifaa vya usalama
Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma
LUKUVI AWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA DAWA ZA KULEVYA
PPAA yatoa elimu matumizi ya Moduli Wiki ya Utumishi wa Umma
Waziri Mkuu Azindua Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini GovESB.
ACT YAITAKA SERIKALI KUONDOA TOZO ZINAZOZUIA BIASHARA KUKUA .
BARAZA LA MADIWANI KINONDONI LAVUNJWA KWA KISHINDO KWA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM.