Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili

IMEELEZWA kuwa hadi kufikia Februari 21, mwaka huu Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa leseni kwa taasisi 2,450 za Daraja la pili.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
26 Feb 2025
Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili

Hayo yamebainishwa leo Februari 26, 2025 mkoani Mtwara na Afisa Mkuu Mwandamizi, Idara ya Usimamizi wa Huduma ndogo za Fedha kutoka BoT, Deogratias Mnyamani wakati akitoa mada ikiwa ni siku ya pili ya semina kwa waandishi wa habari za uchumi.

Amesema hadi sasa maombi yaliyopokelewa ni 3,075 na wamekuwa wakipokea maombi yasiyopungua 18 hadi 20 kwa wiki.

"Biashara ya Huduma ndogo za Fedha imekuwa ikikuwa kwa kasi sana na sasa hivi raia wa kigeni pia wameanza kujitokeza kwa wingi kuomba leseni ili na wao waweze kufanya biashara hii," amesema.

Hata hivyo amesema kuwa, Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 kifungu cha 16(1) kinasema kuwa mtu yeyote nchini haruhusiwi kufanya biashara hiyo bila kuwa na leseni kutoka BoT.

"Kifungu hiki kinasema kuwa mtu atakayefanya hivyo adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili hadi mitano, faini ya sh. Milioni 20 hadi 100 au vyote kwa pamoja.

"Hivyo nitoe wito kwa wanaofanya hivi kuacha mara moja kwani hatua kali zitachukuliwa dhidi yao, na yeyote mwenye taarifa kuhusu wanaofanya hivi atoe taarifa kwetu," amesisisitiza.

Hata hivyo amebainisha hadi kufikia Februari 21, mwaka huu Saccos 970 zimesajiliwa na Vicoba 60,347.

"BoT imekuwa ikiwafutia leseni watoa huduma wasiofuata sheria, kanuni na miongozo inayotolewa pia kwa kushirikiana na jeshi la polisi imefanikiwa kukamata watoa huduma ndogo za fedha wasiokuwa na leseni ya Benki Kuu kwenye mikoa kadhaa nchini.

"Pia imeweza kutoa elimu kwa watoa huduma ndogo za fedha daraja daraja pili, zaidi ya 2,000 mpaka sasa ili kuwapa uelewa juu ya sheria ya huduma ndogo za fedha ya mwaka 2018 na kanuni zake," amesema.

TRA IMEWEZA Kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyabiashara Kujenga Mahusiano na Kutatua Changamoto.

TRA IMEWEZA Kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyabiashara Kujenga Mahusiano na Kutatua Changamoto.

WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU

WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU

JK AIPA PPAA CHANGAMOTO KUOKOA FEDHA ZA SERIKALI KATIKA MIRADI

JK AIPA PPAA CHANGAMOTO KUOKOA FEDHA ZA SERIKALI KATIKA MIRADI

ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AZINDUA KAMPENI YA 'USIKU KAMA MCHANA'KWENYE WILAYA HIYO.

ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AZINDUA KAMPENI YA 'USIKU KAMA MCHANA'KWENYE WILAYA HIYO.

GAVANA TUTUBA: RIBA YA BENKI KUU KUENDELEA KUWA ASILIMIA 6.

GAVANA TUTUBA: RIBA YA BENKI KUU KUENDELEA KUWA ASILIMIA 6.