Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde tarehe 10 mwezi Machi 2025 amekabidhi Kompyuta 50 na Printa 50 kwa Shule za Sekondari za serikali za Dodoma Jiji pamoja na maabara ya kisasa ya Kompyuta kwa Shule ya Sekondari Viwandani na kuahidi kuifanya Dodoma kuwa kinara kwenye matumizi ya teknolojia kwenye kufundishia.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
12 Mar 2025
Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

Mavunde ameyasema hayo katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliyofanyika Shule ya Sekondari Viwandani.

“Tunaipongeza serikali chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu Jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa Tsh 16 bilioni.

Kompyuta hizi na Printa natumai zitachochea ufaulu na kuwajengea uwezo wanafunzi wetu.


Katika Kompyuta hizi tumeweka mitihani yote ya kitaifa kuanzia mwaka 1988-2024 kwa Kidato cha II, IV,VI na QT, vitabu vya ziada na kiada,Simulation za masomo ya Sayansi,video tutorials za masomo mbalimbali na notes za masomo yote“Alisema Mavunde

Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Mbunge Mavunde kwenye sekta ya Elimu na kuitaka Halmashauri ya Jiji Dodoma kuhakikisha inatenga fedha ili kuziunganisha shule zote za Dodoma na Intaneti.

Diwani wa kata ya Viwandani Jaffar Mwanyemba  amemshukuru Mbunge Mavunde kwa ukarabati na kuweka vifaa vya maabara na kuwataka wanafunzi watumie nafasi hiyo kujiongezea maarifa zaidi

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya  Migogoro ya Ardhi Nchini.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.

JAJI WARIOBA: NAPONGEZA CCM KWA HATUA ZAKE DHIDI YA RUSHWA.

JAJI WARIOBA: NAPONGEZA CCM KWA HATUA ZAKE DHIDI YA RUSHWA.

WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI MOROGORO, TANGA WAHIMIZWA KUZINGATIA SHERIA.

WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI MOROGORO, TANGA WAHIMIZWA KUZINGATIA SHERIA.

DKT.NCHIMBI AKEMEA KITENDO CHA MAKADA CCM KUTENGENEZA MATUKIO BINAFSI KWA KIVULI CHA CCM NA KUWALIPA POSHO WANACHAMA.

DKT.NCHIMBI AKEMEA KITENDO CHA MAKADA CCM KUTENGENEZA MATUKIO BINAFSI KWA KIVULI CHA CCM NA KUWALIPA POSHO WANACHAMA.