WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI MOROGORO, TANGA WAHIMIZWA KUZINGATIA SHERIA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI MOROGORO, TANGA WAHIMIZWA KUZINGATIA SHERIA.

Watendaji wa uboreshaji wa Daftari; la Kudumu la Wapiga Kura wameaswa kutekeleza majukumu waliyopewa kwa kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na miongozo itakayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
19 Feb 2025
WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI MOROGORO, TANGA WAHIMIZWA KUZINGATIA SHERIA.

Watendaji wa uboreshaji wa Daftari; la Kudumu la Wapiga Kura wameaswa kutekeleza majukumu waliyopewa kwa kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na
miongozo itakayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Balozi Omari Ramadhan Mapuri wakati akifunga mafunzo ya watendaji wa uboreshaji wa daftari mkoani Morogoro leo Februari 19, 2025.

“Mnapaswa kutekeleza majukumu mliyopewa kwa kuzingatia sheria, kanuni,maelekezo na miongozo itakayotolewa na Tume,” amewaasa watendaji hao ambao wamehudhuria mafunzo ya siku mbili.

Balozi Mapuri ametoa wito kwa watendaji hao kuendelea kutumia muda wao wa ziada kusoma na kupitia maelekezo yote waliyopewa ili kuongeza uelewa zaidi
kuhusu wajibu na majukumu yao wakati wa kutekeleza zoezi lililopo mbele yao.

Akifunga mafunzo kama hayo mkoani Tanga, Mjumbe wa Tume ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari amewataka watendaji hao kusoma katiba na
sheria ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“Someni kwa makini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria ya Uchaguzi, Kanuni za uboreshaji, Maelekezo na Miongozo yote inayotolewa na Tume
ili kazi yenu ifanyike kwa unadhifu na haki,” amesema.

Jaji Asina amewakumbusha watendaji hao juu ya wajibu wao wa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba
itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao kwenye uchaguzi mkuu utakoafanyika mwaka huu.

Uboreshaji wa Daftari  utafanyika mkoani Morogoro na kwenye Mkoa wa Tanga katika Halmashauri za Wilaya ya
Bumbuli, Handeni, Pangani na Mkinga kwa siku saba kuanzia tarehe 01 hadi 07 Machi, 2025 ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa saa 02:00 asubuhi na kufungwa
saa 12:00 jioni.

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya  Migogoro ya Ardhi Nchini.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.

JAJI WARIOBA: NAPONGEZA CCM KWA HATUA ZAKE DHIDI YA RUSHWA.

JAJI WARIOBA: NAPONGEZA CCM KWA HATUA ZAKE DHIDI YA RUSHWA.

DKT.NCHIMBI AKEMEA KITENDO CHA MAKADA CCM KUTENGENEZA MATUKIO BINAFSI KWA KIVULI CHA CCM NA KUWALIPA POSHO WANACHAMA.

DKT.NCHIMBI AKEMEA KITENDO CHA MAKADA CCM KUTENGENEZA MATUKIO BINAFSI KWA KIVULI CHA CCM NA KUWALIPA POSHO WANACHAMA.