![Mwandishi Wetu](https://thedodomapost.co.tz/media/prof/logo.png)
![YANGA SC KUTAFUTA MSHAMBULIAJI TISHIO DIRISHA DOGO.](https://thedodomapost.co.tz/media/news/1701334362.png)
Klabu ya Yanga sc licha ya kuwa miongoni mwa klabu zinazofanya vizuri kwasasa kwenye kikosi chao lakini kuelekea dirisha dogo kocha amependekeza usajili wa maeneo kadhaa ili kuboresha kikosi hiko cha wananchi.
Yanga sc wanahitaji kutafuta natural wingers wenye ubora mkubwa wa kuichezea Yanga sc na kuipambania klabu hiyo kweye michuano mikubwa ndani na nje ya Tanzania.
Lakini pia Yanga sc ipo mawindoni kutafuta mshambuliaji tishio ambaye ataenda kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji katika kikosi hiko cha wananchi.
Ni kweli wanao washambuliaji kadhaa akiwemo Hafiz Konkoni, Kennedy Musonda na Clement Mzize lakini bado klabu inahitaji mshambuliaji hatari zaidi ukizingatia Hafiz tetesi zinaeleza ataachwa katika dirisha dogo la usajili baada ya kuonekana hajakidhi mahitaji ya klabu.
Yapo majina mengi ya wachezaji wanaohusishwa na Yanga sc akiwemo Karamoko Sankara pamoja na Lionel Kateba wote hao wanahusishwa kujiunga na wananchi kwenye dirisha dogo la usajili.
MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO
RAIS DKT SAMIA ATAJWA SHUJAA WA UWEKEZAJI.
DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.
RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.
KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI
DIRA YA TAIFA 2050 NI MAONO YA NCHI SIKU ZA USONI - DKT. BITEKO
WAZIRI BASHE ATANGAZA NEEMA KILIMO CHA UMWAGILIAJI KATAVI.
Vijiji 151 vimebaki nchi nzima kupata huduma ya umeme - Kapinga
WAZIRI MKUU AZINDUA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KIGOMA.
HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.