TICEZA Kuwapa Watanzania Maeneo Bure Kujenga Viwanda | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

TICEZA Kuwapa Watanzania Maeneo Bure Kujenga Viwanda

MAMLAKA ya uwekezaji na maeneo maalum Tanzania (TICEZA) imekuja na motisha ya kutoa maeneo bure kwa wawekezaji wazawa ambao wanataka kuanzisha Viwanda kwa lengo la kutoa ajira kwa Watanzania na kukuza pato la Taifa.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
07 Aug 2025
TICEZA Kuwapa Watanzania Maeneo Bure Kujenga Viwanda

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo,Giliard Terry ameyaeleza hayo Agosti 6 katika Viwanja vya maonyesho ya Wakulima nanenane vilivyopo Nzuguni Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kongamano lilihosu masuala ya uwekezaji kwa wadau mbalimbali wakiwemo wakulima.

Terry amefafanua kuwa kukua kwa Miji nchini imekuwa inaleta   fursa nyingi hasa katika biashara kwa wawekezaji wa ndani ambao wanataka kuwekeza katika Viwanda ambapo Serikali  inataka kuwe na viwanda vya watanzania  100 ili  kuhamasisha kila Mtanzania  anayeweza kujiajiri katika kuelekea mageuzi ya Viwanda.

"Mheshimiwa Rais ametanua wigo wa fursa za kiuchumi kwa Watanzania wote wenye uwezo wa kuwekeza  kwa kujenga Viwanda vya uzalishaji  ambavyo watu watapata vipato vyao wenyewe kwa kutoa ajira kwa Vijana ambao hawana ajira.,"Amesema Mkurugenzi huyo

Aidha amebainisha kuwa  mnamo Agosti  12,Mwaka 2025, saa 3 Asubuhi Jijini Dodoma,Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Mipango na uwekezaji,Profesa Kitila Mkumbo atazindua huduma mpya za Mamlaka hiyo ambapo  kuna  maeneo matano maalum ,ikiwemo.Benjamin Mkapa lililopo Dar, Bagamoyo hekari 150 kwaajili ya viwanda,Dodoma hekari 680 ,eneo la Buzwagi na Kwala lililopo karibu na  Mlandizi lenye hekari 100.

"Tutatangaza kuwa,kwa Mtanzania yeyote mwenye mtaji wa kuanzisha kiwanda na anania na ndoto ya kuwa na Kiwanda afike  kwenye Mamlaka yetu atapewa eneo bure,tunataka watu wajitafutie vipato vyao wenyewe  na kutakuwa na utaratibu wa mchujo kwa watakao jitokeza,"Amesisitiza Terry.

Sanjari na hayo,amebainisha kuwa wataweka utaratibu maalum wa mchujo ili kuondoa ujanjaujanja kwa wale ambao   wadanganyifu ambao wanataka kumiliki maeneo tu lakini hawana uwezo wakumiliki  kiwanda,lengo la Serikali ni kutaka   watanzania wawe wanufaika namba moja katika nchi yao.

Kwa upande wake Charles Tulahi, muwakilishi msaidizi Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) amesema wanafanya kazi kwa ukaribu na Serikali ili kuhakikisha kunakuwa na uzalishaji bora,mazingira bora kwa kila mmoja.

 

Tulahi amesema kuwa mageuzi ya kilimo yanaweza kuondoa  njaa ambapo wamekuwa na miradi ya uwezeshaji wanawake kiuchumi ili kuhakikisha wanakuwa na maisha bora.

"Watanzania wawekeze kwenye Kilimo Kwa sababu kina tija kubwa kutokana na Kuongezeka Kwa Idadi ya watu na teknolojia"Amesema Tulahi

TANESCO YAANZA ZOEZI LA UKAGUZI WA MITA KUBAINI UPOTEVU NA WIZI WA UMEME  UNAOFANYWA NA BAADHI YA WATEJA.

TANESCO YAANZA ZOEZI LA UKAGUZI WA MITA KUBAINI UPOTEVU NA WIZI WA UMEME UNAOFANYWA NA BAADHI YA WATEJA.

SERIKALI  KUTOA  BILIONI 277 KILA MWAKA KUGHARAMIA HUDUMA ZA VVU NA UKIMWI.

SERIKALI KUTOA BILIONI 277 KILA MWAKA KUGHARAMIA HUDUMA ZA VVU NA UKIMWI.

VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI.

VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI.

TANESCO YAZINDUA MFUMO WA UPOKEAJI TAARIFA KWA SIRI WATAKA WANANCHI KUUTUMIA ILI KURIPOTI VITENDO VYA UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA SHIRIKA.

TANESCO YAZINDUA MFUMO WA UPOKEAJI TAARIFA KWA SIRI WATAKA WANANCHI KUUTUMIA ILI KURIPOTI VITENDO VYA UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA SHIRIKA.

ELAF YAITAKA SERIKALI KUUNDA CHOMBO MAALUMU CHA KUSHUGHULIKIA UPOTEVU WA WATU NCHINI.

ELAF YAITAKA SERIKALI KUUNDA CHOMBO MAALUMU CHA KUSHUGHULIKIA UPOTEVU WA WATU NCHINI.