INEC YAWATAKA WAZALISHAJI MAUDHUI MTANDAO KUZINGATIA WELEDI NA TAALUMA ILI KULINDA AMANI YA NCHI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

INEC YAWATAKA WAZALISHAJI MAUDHUI MTANDAO KUZINGATIA WELEDI NA TAALUMA ILI KULINDA AMANI YA NCHI.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wazalishaji wa maudhui mtandaoni kuzalisha  maudhui  yatakayo wahamisha wananchi kujitokeza katika kupiga kura kwa kuwa ni haki yao kikatiba na si kuweka maudhui yatakayohamasisha uvunjifu wa amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
03 Aug 2025
INEC YAWATAKA WAZALISHAJI MAUDHUI MTANDAO KUZINGATIA WELEDI NA TAALUMA ILI KULINDA AMANI YA NCHI.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wazalishaji wa maudhui mtandaoni  kuzalisha  maudhui  yatakayo wahamisha wananchi kujitokeza katika kupiga kura kwa kuwa ni haki yao kikatiba na si kuweka maudhui yatakayohamasisha uvunjifu wa amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.

Wito huo ameutoa leo Agosti 3,2025 akifungua  wakati wa mkutano wa Kitaifa wa Tume hiyo na wazalishaji wa maudhui mtandaoni kilichofanyima katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo amewataka waandaji hao kuandika habari za kweli zinasosimamia sheria kanuni na maadili.

"Hakikisheni taarifa zinazopandishwa katika kurasa zenu zinasimamia weledi ili kuepuka uvunjifu wa amani nchini Nawakumbusha juu ya umuhimu wa kuepuka matumizi mabaya ya akili unde ambayo inatumiwa na baadhi ya watu wenye nia ovu kusambaza habari za upotoshaji hasa kupitia mitandao ya kijamii," amesema.

 

Aidha ameongeza kuwa ni vema wazalishaji kutengeneza maudhui yatakayo wahamasisha vijana na watumiaji wa teknolojia kupitia mitandao ya kijamii kupata hamasa na kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi unatarajiwa kufanyika mnamo  Oktoba mwaka huu.

Awali akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu na ushiriki wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhan Kailima amesema Tume inatarajia vyombo vyahabari vitatumia kalamu zao na nyenzo walizonanzo kuhubiri amani katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi lakini pia kutoa nafasi sawa kwa wagombea wa vyama vyote katika vyombo vyao vya habari.

"Tume imejiwekea utaratibu wa kuvishirikisha vyombo vya habari katika mchakato mzima wa uendeshaji wa uchaguzi huu ili kuweka uwazi na kuhakikisha wanashiriki kikamilifu, tunawaomba kutumia nafasi na fursa mlizonazo kuhakikisha kunakuwepo na taarifa za mara kwa mara za kuelezea kinachoendelea kuhusu uchaguzi, "Amesema Kailima

ACT WAJIPANGA KUIONDOA CCM MADARAKANI UCHAGUZI MKUU 2025.

ACT WAJIPANGA KUIONDOA CCM MADARAKANI UCHAGUZI MKUU 2025.

Chama cha National League for Democracy (NLD) Klmezinduwa  Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya  kwa Mwaka 2025

Chama cha National League for Democracy (NLD) Klmezinduwa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya kwa Mwaka 2025

KIBAHA YAANZA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

KIBAHA YAANZA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

KAILIMA ASEMA TUME ITAFANYA KAZI KWA KARIBU NA WAANDISHI WA HABARI KIPINDI CHOTE CHA UCHAGUZI MKUU 2025.

KAILIMA ASEMA TUME ITAFANYA KAZI KWA KARIBU NA WAANDISHI WA HABARI KIPINDI CHOTE CHA UCHAGUZI MKUU 2025.

WAANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUHAMASISHA USHIRIKI WA WANANCHI KUPIGA KURA

WAANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUHAMASISHA USHIRIKI WA WANANCHI KUPIGA KURA