

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wazalishaji wa maudhui mtandaoni kuzalisha maudhui yatakayo wahamisha wananchi kujitokeza katika kupiga kura kwa kuwa ni haki yao kikatiba na si kuweka maudhui yatakayohamasisha uvunjifu wa amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wazalishaji wa maudhui mtandaoni kuzalisha maudhui yatakayo wahamisha wananchi kujitokeza katika kupiga kura kwa kuwa ni haki yao kikatiba na si kuweka maudhui yatakayohamasisha uvunjifu wa amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.
Wito huo ameutoa leo Agosti 3,2025 akifungua wakati wa mkutano wa Kitaifa wa Tume hiyo na wazalishaji wa maudhui mtandaoni kilichofanyima katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo amewataka waandaji hao kuandika habari za kweli zinasosimamia sheria kanuni na maadili.
"Hakikisheni taarifa zinazopandishwa katika kurasa zenu zinasimamia weledi ili kuepuka uvunjifu wa amani nchini Nawakumbusha juu ya umuhimu wa kuepuka matumizi mabaya ya akili unde ambayo inatumiwa na baadhi ya watu wenye nia ovu kusambaza habari za upotoshaji hasa kupitia mitandao ya kijamii," amesema.
Aidha ameongeza kuwa ni vema wazalishaji kutengeneza maudhui yatakayo wahamasisha vijana na watumiaji wa teknolojia kupitia mitandao ya kijamii kupata hamasa na kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi unatarajiwa kufanyika mnamo Oktoba mwaka huu.
Awali akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu na ushiriki wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhan Kailima amesema Tume inatarajia vyombo vyahabari vitatumia kalamu zao na nyenzo walizonanzo kuhubiri amani katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi lakini pia kutoa nafasi sawa kwa wagombea wa vyama vyote katika vyombo vyao vya habari.
"Tume imejiwekea utaratibu wa kuvishirikisha vyombo vya habari katika mchakato mzima wa uendeshaji wa uchaguzi huu ili kuweka uwazi na kuhakikisha wanashiriki kikamilifu, tunawaomba kutumia nafasi na fursa mlizonazo kuhakikisha kunakuwepo na taarifa za mara kwa mara za kuelezea kinachoendelea kuhusu uchaguzi, "Amesema Kailima
ACT WAJIPANGA KUIONDOA CCM MADARAKANI UCHAGUZI MKUU 2025.
EQUITY BANK YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA BAJAJ KWA AJILI YA KUWASAIDIA WAKULIMA
Kilundumya Aipongeza e-GA Kwa Kuimarisha Ushirikiano na Sekta ya Kilimo Kuleta Mapinduzi Kidigitali.
WIZARA YA NISHATI ENDELEENI KUSIMAMIA UFANISI WA MIRADI YA NISHATI- DED MKALAMA.
Chama cha National League for Democracy (NLD) Klmezinduwa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya kwa Mwaka 2025
TADB Yawawezesha Wakulima Wadogo Mikopo Yenye Dhamana Nafuu.
MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025.
Coop Bank Imejipanga Kutoa Huduma Maalum kwa Washiriki wa Maonesho ya NaneNane.
WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME
VIONGOZI WA DINI WAASWA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YAO YA NDANI PASIPO KUZUA TAHARUKI ILI KULINDA AMANI YA NCHI.