TAWOMA YATOA RAI KWA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZILIZOPO KWENYE SEKTA YA MADINI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Nishati

TAWOMA YATOA RAI KWA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZILIZOPO KWENYE SEKTA YA MADINI.

CHAMA cha wanawake wachimbaji madini nchini (TAWOMA) kimetoa fursa kwa vijana wanaohitaji kujishughulisha katika uchimbaji kuweza kujifunza na kujitengenezea ajira ili kuongeza kipato chao binafsi na kuchangia katima pato la Taifa.

Na SOPHIA KINGIMALI
By Na SOPHIA KINGIMALI
14 Jul 2025
TAWOMA YATOA RAI KWA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZILIZOPO KWENYE SEKTA YA MADINI.

CHAMA cha wanawake wachimbaji madini nchini (TAWOMA) kimetoa fursa kwa vijana wanaohitaji kujishughulisha katika uchimbaji kuweza kujifunza na kujitengenezea ajira ili kuongeza kipato chao binafsi na kuchangia katima pato la Taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuhitimishwa kwa maonesho ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba Katibu Mkuu wa TAWOMA Salma Ernest amesema wameanzisha  programu ya vijana ili kuwasaidia kujiajiri kupitia sekta ya madini.

"Mpaka sasa kupitia program hiyo vijana zaidi ya 60 wamepata mafunzo kupitia sekta ya madini pamoja na wale waliomaliza kusoma chuo  cha uchakataji madini kilichopo  mkoani Arusha",Amesema.

Aidha ameongeza kuwa wanavijana ambao mamemaliza chuo cha madini cha Arusha ambapo wao ni wabunifu na wamepitia kujifunza uongezaji thamani madini ya vito ikiwa ni pamoja na kutengeneza vitu mbalimbali kama picha,na bidhaa mbalimbali za kuvaa wanawake na wanaume.

"Vijana hao wameongeza ujuzi wa kukata madini katika maumbo mbalimbali ambapo sasa wanauza kupitia duka ambalo lipo mtaa wa undali jijini Dar es salaam na bidhaa hapo zinapatikna kwa bei nafuu",amesema.

Kwa upande wake STANLEY EDward kutoka kituo cha jiolojia amesema watanzania wengi hawajui aina za madini mbalimbali yaliyopo nchini na fursa zitokanazo na madini hayo.

"Watanzania wengi hawajui aina za madini yaliyopo hapa nchini wengi wamezoea madini kama Tanzanite,dhahabu,silver,almasi,rubi,diamond lakini ukweli ni kwamba kuna madini mengi nchini na yanatoa fursa kwa vijana kuweza kujiajili",amesema.

Ameongeza kuwa kituo chao cha jiolojia kimekuwa kikitoa mafunzo kwenye uongezaji thamani kama ukataji na ung'arishaji wa bidhaa tofauti zinazotokana na madini hivyo ametoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa hizo.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKABIDHI TUZO YA UMAHIRI KWA MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO WIZARA YA NISHATI.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKABIDHI TUZO YA UMAHIRI KWA MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO WIZARA YA NISHATI.

TANZANIA  INA UMEME WA KUTOSHA – DKT. BITEKO

TANZANIA INA UMEME WA KUTOSHA – DKT. BITEKO

PURA MBIONI KUCHIMBA VISIMA VITATU VYA GESI ASILIA MKOANI MTWARA.

PURA MBIONI KUCHIMBA VISIMA VITATU VYA GESI ASILIA MKOANI MTWARA.

RAIS MWINYI ATEMBELEA BANDA LA NISHATI MAONESHO YA SABASABA

RAIS MWINYI ATEMBELEA BANDA LA NISHATI MAONESHO YA SABASABA

Wenye malori watakiwa kuweka vifaa vya usalama

Wenye malori watakiwa kuweka vifaa vya usalama