TUTAENDELEA KUINADI TANZANIA KWA NGUVU ZOTE EXPO 2025 JAPAN- MWAMWAJA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Utalii

TUTAENDELEA KUINADI TANZANIA KWA NGUVU ZOTE EXPO 2025 JAPAN- MWAMWAJA.

Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Bw. Ernest Mwamwaja amesema Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia bodi hiyo itaendelea kuitangaza Tanzania kwa nguvu zote katika maonesho ya Uchumi na Biashara maarufu kama Expo Osaka 2025 yanayofanyika nchini Japan.

na Hamis Dambaya.
By na Hamis Dambaya.
05 May 2025
TUTAENDELEA KUINADI TANZANIA KWA NGUVU ZOTE EXPO 2025 JAPAN- MWAMWAJA.

Bwana Mwamwaja ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumzia kuhusu  mwenendo wa ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo yanayoratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara-TANTRADE yaliyoanza Aprili 13 mwaka huu na  yanatarajiwa kuendelea  kwa muda  wa miezi 6 ambapo yatamalizika  mwezi Oktoba mwaka huu.

Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa hadi sasa Tanzania imefanikiwa kuvutia watembeleaji wengi katika banda lake na watu wanaopata taarifa kuhusu vivutio vilivyopo wameonesha nia ya kuvitembelea.

“Tunafarijika kuona kwamba idadi ya watembeleaji katika banda letu ni kubwa na wengi wao wanaonesha dhamira ya dhati ya kutaka kufika Tanzania baada ya kunadi vivutio vyetu, kwetu sisi kama wizara haya ni mafanikio makubwa”,alisema Bw. Mwamwaja.

Katika wiki hii ya Utalii iliyoanza tarehe 25 Aprili 2025, ambayo kwa upande wa Tanzania ilizinduliwa na Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mhe. Baraka Luvanda, Tanzania imeitumia wiki hiyo kutangaza fursa za utalii zilizopo.

Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii zikiwemo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) yameendela kutumia fursa hiyo kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika maeneo yao.

Akizungumzia ushiriki katika maonesho hayo Naibu Kamishna wa Uhifadhi  TANAPA,  Bw. Massana Mwishawa ameelezea kuwa shirika hilo  limetangaza maeneo ya uwekezaji hasa katika huduma za malazi na shughuli za utalii.

Kwa upande wake, Afisa Uhifadhi Mkuu upande wa masoko kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro  Bw  Michael Makombe amesema NCAA imekuwa ikitumia   fursa hiyo kuwakaribisha wageni  kutembelea hifadhi hiyo na kujionea fursa mbalimbali zilizopo.

Akizungumzia ushiriki wa TAWA katika maonesho hayo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa mamlaka hiyo Bi. Lilian Wawa  amesema kutoka pamoja na kunadi utalii, OSAKA EXPO 2025 inatumika kushawishi uwekezaji wa Kampuni za kimataifa katika mazao ya utalii wa Uwindaji na wa picha.

Maonesho ya Osaka EXPO yanayoendelea nchini Japan yanatarajiwa kutembelewa na wageni wasiopungua milioni 28 waoneshaji kutoka zaidi ya nchi 160 duniani wanashiriki.

MKURUGENZI WA MASOKO TTB AELEZA FURSA INAYOWEZA KUPATA TANZANIA KUTOKA  JAPAN KATIKA ELIMU YA UTALII NA UHIFADHI

MKURUGENZI WA MASOKO TTB AELEZA FURSA INAYOWEZA KUPATA TANZANIA KUTOKA JAPAN KATIKA ELIMU YA UTALII NA UHIFADHI

MENEJIMENTI YA NCAA YAPATA MAFUNZO YA KUBORESHA UTENDAJI KAZI

MENEJIMENTI YA NCAA YAPATA MAFUNZO YA KUBORESHA UTENDAJI KAZI

BALOZI LUVANDA AONGOZA UJUMBE WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAKALA WA UTALII NCHINI JAPAN

BALOZI LUVANDA AONGOZA UJUMBE WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAKALA WA UTALII NCHINI JAPAN

WAJUMBE WA MKUTANO WA BARAZA LA VIWANJA VYA NDEGE AFRIKA WAFURAHIA VIVUTIO VYA UTALII NGORONGORO.

WAJUMBE WA MKUTANO WA BARAZA LA VIWANJA VYA NDEGE AFRIKA WAFURAHIA VIVUTIO VYA UTALII NGORONGORO.

DKT. DORIYE AONGOZA MENEJIMENTI YA NCAA KIAPO CHA AHADI YA UADILIFU KWA VIONGOZI WA UMMA.

DKT. DORIYE AONGOZA MENEJIMENTI YA NCAA KIAPO CHA AHADI YA UADILIFU KWA VIONGOZI WA UMMA.