

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Dkt. Elirehema Doriye ameiongoza Menejimenti ya Mamlaka hiyo kupata mafunzo katika nyanja mbalimbali ili kuendana na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi kulingana na wakati.
Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku tatu jijini Arusha kuanzia tarehe 5-7 Mei, 2025 yalijikita katika sheria ya maadili ya viongozi wa Umma, sifa za uongozi, utunzaji wa siri na nyaraka za Serikali, uedeshaji wa ofisi za Umma, afya ya akili na akili hisia
“Mafunzo mahala pa kazi yanaimarisha utendaji kazi hasa katika utekelezaji wa majukumu, dunia inabadilika kwa sasa kuna masuala ya akili hisia “emotional intelligence”, akili mnemba “artificial intelligence”, maadili katika utumishi wa Umma, uendeshaji wa ofisi za umma na kuongeza ufanisi katika kuhudumia wateja wetu, sasa ili kuongeza ufanisi katika masuala haya tuna wajibu wa kuwa na mafunzo ya mara kwa mara ambayo pia yatatusaidia kuongoza tunaowasimamia ” alisisitiza Dkt. Doriye.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege