

Wajumbe zaidi ya 137 kutoka nchi mbalimbali barani Afrika waliokuwa wakihudhuria mkutano mkuu wa 73 wa Baraza la Viwanja vya Ndege Afrika leo Aprili 30, 2025, wamefanya ziara katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na kufurahia vivutio vya utalii vilivyoko katika hifadhi hiyo
Ziara hiyo ambayo imefanyika baada ya kumalizika kwa Mkutano mkuu wa Baraza hilo uliofanyika jijini Arusha kuanzia Aprili 24 hadi 30, 2025 imelenga kuunga mkono jitihada za Serikali na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kuhamasisha utalii na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Ngorongoro na maeneo mengine ya nchi.
Akizungumza wakati wa kupokea ugeni huo, Afisa uhifadhi Mkuu kutoka Idara ya Huduma za Utalii na Masako Peter Makutian, amesema kuwa kutokana na jitihada zinazofanywa na Mamlaka za kuhamasisha utalii ndani na nje ya nchi wamekuwa wakipokea makundi makubwa ya watalii ambao wamekuwa wakivutiwa kutembelea vivutio mbalimbali ikiwemo kreta ya Ngorongoro inayotajwa kuwepo kwenye maajabu saba ya Asili barani Afrika.
“Leo tumepokea wageni kutoka baraza la viwanja vya ndege ambao wamevutiwa kuja kutembelea vivutio vya utalii Hifadhi ya Ngorongoro, tunaamini ujio wa ugeni huu utaendelea kuhamasisha utalii kutoka kwa wageni wa ndani na nje nchi, wametembelea kreta ya Ngorongoro na maeneo mengine ambapo wamejionea Wanyama mbalimbali, vivutio vya malikale, uoto wa asili na mandhari mbalimbali ” Alisema Makutian
Kwa upande Bi. Violeth Mfuko ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Viola Tours & Travel limited iliyoratibu ziara hiyo alieleza kuwa, vivutio ambavyo vinapatikana ndani ya Eneo la Ngorongoro hasa Bonde la Kreta na maeneo mengine ambayo yamekuwa kivutio cha kipekee kwa watalii wengi kuwa na shauku kubwa ya kutembelea maeneo hayo kutokana na uzuri wake wa asili na kuwa eneo la urithi wa dunia lenye uhifadhi endelevu.
Katika hatua nyingine, NCAA imetumia fursa hiyo kuhamasisha wageni wa baraza hilo kulipigia kura eneo la Hifadhi ya Ngorongoro linalowania tuzo ya kuwa Kivutio Bora cha Utalii Barani Afrika kupitia tuzo ambazo zinaratibiwa na mtandao wa World Travel Awards.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege