BADO TUNAMUHITAJI POLEPOLE KWA MKURUGENZI WA UPELELEZI- POLISI | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

BADO TUNAMUHITAJI POLEPOLE KWA MKURUGENZI WA UPELELEZI- POLISI

Jeshi la Polisi nchini Tanzania kupitia kwa Msemaji wake DCP David Misime limesisitiza kuwa bado linaendelea kumsubiri Ndugu Humphrey Polepole ili aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya jinai ili atoe maelezo kuhusu tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia Mitandao yake ya Kijamii.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
06 Oct 2025
BADO TUNAMUHITAJI POLEPOLE KWA MKURUGENZI WA UPELELEZI- POLISI

Jeshi la Polisi nchini Tanzania kupitia kwa Msemaji wake DCP David Misime limesisitiza kuwa bado linaendelea kumsubiri Ndugu Humphrey Polepole ili aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya jinai ili atoe maelezo kuhusu tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia Mitandao yake ya Kijamii.

Ikumbukwe kuwa Jumatatu Septemba 15, 2025 Jeshi la Polisi lilisema kuwa limefungua jalada la uchunguzi na linaendelea kuchunguza tuhuma mbalimbali ambazo amekuwa akizitoa kada huyo wa Chama Cha Mapinduzi CCM.

"Tuhuma ambazo ametoa na anaendelea kuzitoa kulingana na jinsi alivyozielezea zinaashiria uwepo wa makosa ya kijinai na kwa mujibu wa sheria zinahitaji ushahidi wa kuzithibitisha zitakapo wasilishwa mahakamani.

Tuhuma hizo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya kijamii, baada ya kufungua jalada na kuanza uchunguzi, Jeshi la Polisi mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa maelezo au ushahidi na vielelezo vitakavyo thibitisha tuhuma hizo ili kuwezesha hatua zingine za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria na ndivyo utaratibu wa kisheria ulivyo" Taarifa hiyo ya Polisi ilieleza.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi limeeleza kuona taarifa zinazosambazwa kwenye Mitandao ya kijamii na ndugu zake kuwa Mtu huyo ametekwa usiku wa kuamkia Oktoba 06, 2025 na kueleza kuwa tayari wameanza kufanyia kazi taarifa husika ili kupata ukweli wa madai ya kutekwa kwake.

Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”

Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”

MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.

MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.

DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”

DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”

VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI

VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI

VIJANA WATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTIMIZA MATARAJIO YAO

VIJANA WATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTIMIZA MATARAJIO YAO