WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.

Wazee wa Mkoa wa Dodoma waaswa kuhamasisha jamii kujitokeza Oktoba 29,2025 kupiga kura pamoja na kuhakikisha wanasimamia vijana na kuwasihi kulinda amani ya nchi yetu.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
09 Oct 2025
WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.

Wazee wa Mkoa wa Dodoma waaswa kuhamasisha jamii kujitokeza Oktoba 29,2025 kupiga kura pamoja na kuhakikisha wanasimamia vijana na kuwasihi kulinda amani ya nchi yetu.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule wakati akizungumza na Wazee hao leo Oktoba 09 juu ya umuhimu wao wa kuhamasisha jamii kujitokeza kupiga kura.

Aidha amesema kuwa ni jukumu la Kila mwananchi kuchagua viongozi wenye tija na maendeleo hivyo amewasihi wazee kuwa mstari wa mbele kwenye suala la uchaguzi kwani maendeleo yaliyofanywa na Serikali yanaonekana dhahiri.

Aidha amesema Dodoma ya miaka 10 iliyopita si sawa na Dodoma ya sasa kwani hata hadhi ya viwanja imeongezeka na kila mtu amekuwa akivutiwa na Dodoma hivyo anaipongeza Serikali kwa kufanya Dodoma kuwa ya kuvutia.

"Dodoma ya sasa si kama ya zamani Dodoma sasa inavutia na ni kimbilio la watanzania na wageni wa kimataifa kuwekeza Dodoma na hii ni kutokana na mabadiliko makubwa yaliyofanywa na Serikali"Amesema Senyamule

Sanjari na hayo amesema kuwa Serikali imeamua kutoa Elimu juu ya magomjwa yasiyoambukizwa ili waweze kuhakikisha wazee wanakuwa imara kwenye Afya Kwa kufanya mazoezi na Kuzingatia mlo mzuri kulingana na umri wao.

"Kupitia nyie tutaweza kujua changamoto mlizonazo na kuweza kuhakikisha tunazitatua kwani wazee ni tunu ya taifa hili"Ameongeza Senyamule

Wazee hao nao walipata nafasi ya kuelezea changamoto zao Kwa Mkuu wa Mkoa wanazokumbana nazo kwenye huduma za Kijamii ikiwemo hospitali ambapo Mzee Bakari Chaurembo ameiomba Serikali kuwaangalia Kwa jicho la 3 Kwa kuhakikisha wanapatiwa Bima ya Afya ili waweze kupata huduma kwa urahisi na wakati kipindi wanapokwenda kwenye vituo vya Afya.

Akijibu hoja za wazee hao Mkuu wa Mkoa amesema atahakikisha anashughulikia changamoto zote ikiwemo huduma mbovu Kwa wazee kwenye vituo vya Afya,pamoja na kuboresha miundombinu  kama barabara ili kuweza kukidhi matakwa ya Wazee hao.

"Kwenye ishu ya Wazee kutopanga foleni siku ya kupiga kura tutaliwasilisha Kwa TUME ya uchaguzi ili muweze kutengenezewa utaratibu mzuri"Amesisitiza Senyamule

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya  VSOMO ya VETA

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya VSOMO ya VETA

WENYE ULEMAVU WAHAMASISHA KUJITOKEZA KUWACHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTETEA MASLAHI YAO

WENYE ULEMAVU WAHAMASISHA KUJITOKEZA KUWACHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTETEA MASLAHI YAO