TAWA YATUMIA MAONESHO YA 31 YA NANE NANE 2025 KUELIMISHA UMMA NA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII | The Dodoma Post
The Dodoma Post Utalii

TAWA YATUMIA MAONESHO YA 31 YA NANE NANE 2025 KUELIMISHA UMMA NA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), kupitia Kanda ya Kaskazini, inaendelea kutumia jukwaa la Maonesho ya Nane Nane 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Nane Nane mkoani Arusha kuwafikia Watanzania kwa kuwapatia elimu kuhusu uhifadhi, utalii na fursa za uwekezaji katika maeneo yake ya usimamizi.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
04 Aug 2025
TAWA YATUMIA MAONESHO YA 31 YA NANE NANE 2025  KUELIMISHA UMMA NA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), kupitia Kanda ya Kaskazini, inaendelea kutumia jukwaa la Maonesho ya Nane Nane 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Nane Nane mkoani Arusha kuwafikia Watanzania kwa kuwapatia elimu kuhusu uhifadhi, utalii na fursa za uwekezaji katika maeneo yake ya usimamizi.

Kupitia ushiriki wake ndani ya banda la pamoja la Wizara ya Maliasili na Utalii, TAWA inatoa taarifa na elimu kwa umma kuhusu vivutio vya utalii vilivyoko Kanda ya Kaskazini na maeneo mengine nchini, sambamba na fursa za uwekezaji katika sekta ya uhifadhi. Maonesho hayo yaliyoanza rasmi tarehe 1 Agosti 2025 yamekuwa jukwaa muhimu la kuwasiliana moja kwa moja na wananchi.

Mbali na utoaji wa elimu, TAWA kwa kushirikiana na wadau wake imewavutia wananchi kwa kuonesha Wanyamapori hai wakiwemo Simba, Fisi na Mamba ambao wamekuwa kivutio kikubwa kwa wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Arusha wanaotembelea banda la Maliasili na Utalii.

Takwimu za awali zinaonesha kuwa kufikia tarehe 3 Agosti 2025, zaidi ya wananchi 350 wamepokea huduma ya elimu na maelezo kutoka kwa wataalamu wa TAWA. Kazi ya uelimishaji na uhamasishaji inaendelea hadi kilele cha maonesho hayo mnamo tarehe 8 Agosti 2025.

TAWA inahimiza wananchi wote kutembelea banda la Maliasili na Utalii ili kupata taarifa sahihi, kujifunza kuhusu utalii wa ndani, na kufahamu nafasi walizonazo katika kulinda urithi wa taifa na kuchangamkia fursa za uwekezaji zinazotolewa.

ARUSHA YAJIVUNIA ONGEZEKO LA WATALII KUPITIA FILAMU YA THE  ROYAL TOUR.

ARUSHA YAJIVUNIA ONGEZEKO LA WATALII KUPITIA FILAMU YA THE ROYAL TOUR.

AJIRA ZA MOJA KWA MOJA KATIKA SEKTA YA UTALII ZIMEONGEZEKA.

AJIRA ZA MOJA KWA MOJA KATIKA SEKTA YA UTALII ZIMEONGEZEKA.

IDADI YA WATALII WA NDANI WALIOTEMBELEA MKOA WA TABORA IMEONGEZEKA.

IDADI YA WATALII WA NDANI WALIOTEMBELEA MKOA WA TABORA IMEONGEZEKA.

TANZANIA YAENDELEA KUTANGAZA NA KUKUZA KISWAHILI NA UTAMADUNI WAKE KIMATAIFA

TANZANIA YAENDELEA KUTANGAZA NA KUKUZA KISWAHILI NA UTAMADUNI WAKE KIMATAIFA