

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Dkt. Elirehema Doriye leo tarehe 5 Mei, 2025 ameiongoza Menejimenti ya Mamlaka hiyo kwenye zoezi la kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma katika hafla iliyofanyika ofisi za NCAA zilizopo Arusha.
Akizungumza baada ya kiapo hicho Dkt Doriye ameeleza kuwa menejimenti ya NCAA inaonesha dhamira ya pamoja ya kuzingatia maadili, uwajibikaji na uadilifu katika kutekeleza majukumu ya kuhifadhi, utalii, maendeleo ya jamii na urithi wa kipekee wa asili na utamaduni katika hifadhi ya Ngorongoro kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.
Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Kaskazini Gerald Mwaitebele ameeleza kuwa kiapo cha maadili kwa viongozi wa umma kinafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995 ambapo Sekretarieti ya Maadili ina jukumu la kukuza na kusimamia Maadili ya Viongozi wa Umma nchini ili kuhakikisha kwamba Viongozi wa Umma wanakuwa na tabia na mwenendo wa kimaadili.
Zoezi la kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma kwa menejimenti ya
NCAA kimeenda sambamba na utoaji wa mafunzo mbalimbali ambayo yanalenga kuwaelimisha viongozi hao kuhusu miongozo ya maadili kwa viongozi wa umma ili kuboresha utendaji kazi wa Menejimenti ya NCAA kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji, uadilifu na uongozi bora.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege