ONANA AKIRI KIWANGO CHAKE KUSHUKA ALIPOTUA MAN UNITED | The Dodoma Post
The Dodoma Post Michezo

ONANA AKIRI KIWANGO CHAKE KUSHUKA ALIPOTUA MAN UNITED

Mlinda mlango wa Manchester United, AndreOnana amekiri kiwango chake kimeshuka tangu alipotua manchesterunited , lakini amewatoa hofu mashabiki kwa kueleza kuwa soon mambo yatakuwa sawa.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
20 Dec 2023
ONANA AKIRI KIWANGO CHAKE KUSHUKA ALIPOTUA MAN UNITED

Mcamerooni huyo, mwenye umri wa miaka 27, alitua Man United akitokea Inter Milan wakati wa dirisha lililopita la uhamisho wa majira ya kiangazi huko Ulaya, kama chaguo la kwanza baada ya David de Gea kuruhusiwa kuondoka bure kwenye kikosi hicho.

#Andre amekutana na wakati mgumu, akiruhusu mabao 39 katika mechi 25 alizochezea timu hiyo msimu huu, ikiwamo mabao 15 katika mechi sita tu za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa #Ulaya.

Baada ya kusemwa sana kuhusu kiwango chake, #Onana aliwajibu wanaomkosoa kwa kusema "kipa bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita ghafla tu amekuwa wa hovyo duniani.

"Kama nitazungumzia msimu wangu hadi sasa hapa #ManUnited, sifurahii kwa sababu ningeweza kufanya vizuri zaidi, najua naweza kufanya vizuri zaidi ya hiki kinachotokea sasa.

"Kila kitu ni cha kupita. Najua nitakuwa sawa. Kama sio leo, itakuwa kesho, kama si kesho basi itakuwa siku inayofuata baada ya kesho."

GRAND BUNGE  BONANZA KUFANYIKA  JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.

GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.

DODOMA YAELEKEA IRINGA KWA KISHINDO MASHINDANO YA UMISSETA.

DODOMA YAELEKEA IRINGA KWA KISHINDO MASHINDANO YA UMISSETA.

Mashindano ya Polisi Jamii  Kuimarisha mahusiano kati ya Polisi na Wananchi

Mashindano ya Polisi Jamii Kuimarisha mahusiano kati ya Polisi na Wananchi

Simba SC Yajivunia Kuendelea na Vita Baada ya Kudondosha Pointi Moroco

Simba SC Yajivunia Kuendelea na Vita Baada ya Kudondosha Pointi Moroco

ALLY KAMWE mikononi mwa Polisi, yataja chanzo

ALLY KAMWE mikononi mwa Polisi, yataja chanzo