RITA Yaendelea Kuupiga Mwingi Sabasaba | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

RITA Yaendelea Kuupiga Mwingi Sabasaba

Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) imesajili zàidi ya Watanzania elfu tatu waliojitikeza kupata huduma kwenye maonyesho ya 47 ya Kimataifa ya biashara SabaSaba ambapo elfu mbili kati yao wamesajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa hapo hapo.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
10 Jul 2023
RITA Yaendelea Kuupiga Mwingi Sabasaba

Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) imesajili zàidi ya Watanzania elfu tatu waliojitikeza kupata huduma kwenye maonyesho ya 47 ya Kimataifa ya biashara SabaSaba ambapo elfu mbili kati yao wamesajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa hapo hapo.

Hayo yamebainishwa July 9, 2023 jijini Dar es Salaam na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Frank Kanyusi alipokuwa akishuhudia baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye banda hilo ambalo lipo kwenye Maonesho hayo yanayoendelea nchini. 

"Tunatoa huduma zetu zote na tunaomba watanzania wazidi kujitokeza kwa wingi maana tumejipanga vizuri kuwahudumia watanzania,tunatoa vyeti hapa hapa kwenye maonesho na tayari wananchi zaidi ya elfu mbili tumewapatia vyeti na tunatarajia wazidi kujitokeza ili wasipitwe na fursa hii,” amesema Kanyusi.

Amesema jumuku la RITA ni kutoa huduma bora kwa wananchi wake hasa ikiwemo cheti cha kuzaliwa kupitia maonesho hayo, elimu kuhusu mirathi, kuandika na kuhifadhi wosia  na wametumia nafasi hiyo kuwasaidia Watanzania waweze kusaidiwa kwa haraka kupata cheti na urahisi kupata cheti cha kuzaliwa.

Aidha baadhi ya wananchi waliojitokeza kupata huduma mbali mbali wamesifu utendaji kazi wa RITA na kusifu jitihada walizozifanya kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa ndani ya siku moja.

"Tunawapongeza maana sio kazi rahisi kuwahudumia watu wengi kiasi hiki, hii inaonesha namna walivyojipanga vizuri mimi nimejiandikisha na nimepata cheti," amesema Leonard Cleopatra mmoja ya wananchi waliojitokeza kupata Huduma.

RITA inaendelea kutoa Huduma ya kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa, elimu ya kuandika na kuhifadhi wosia kwenye Maonesho ya 47 ya biashara ya kimataifa hadi Julai 13, 2023.

MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.

MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.

HANANJA AWAONYA VIONGOZI WA DINI WANAOTUMIA MAJUKWAA YA DINI KUPOTOSHA UMMA.

HANANJA AWAONYA VIONGOZI WA DINI WANAOTUMIA MAJUKWAA YA DINI KUPOTOSHA UMMA.

Waziri Mhagama amewataka kina Mama kuwa makini na Bidhaa Wanazotumia wakati wa Hedhi.

Waziri Mhagama amewataka kina Mama kuwa makini na Bidhaa Wanazotumia wakati wa Hedhi.

DMI YATOA ELIMU YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MAJINI JIJINI DODOMA

DMI YATOA ELIMU YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MAJINI JIJINI DODOMA

Makamu wa Rais Dkt.Mpango Ametoa Wito Kwa Wadau wa Mazingira Kuendeleza Utunzaji wa Mazingira.

Makamu wa Rais Dkt.Mpango Ametoa Wito Kwa Wadau wa Mazingira Kuendeleza Utunzaji wa Mazingira.