

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tanga imetoa onyo kali kwa wananchi wote wenye nia ovu ya kuvunja amani katika kipindi cha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, ikisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayejihusisha na vitendo hivyo.
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tanga imetoa onyo kali kwa wananchi wote wenye nia ovu ya kuvunja amani katika kipindi cha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, ikisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayejihusisha na vitendo hivyo.
Onyo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Buriani, wakati akizungumza na waandishi wa habari akiwa ameambatana na Kamati ya Amani pamoja na viongozi wa vyama vya siasa mkoani humo.
Balozi Batilda amesema serikali haitasita kuchukua hatua kwa mtu yeyote atakayehatarisha utulivu na amani ya mkoa huo siku ya uchaguzi.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani na kuacha kujihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani.
Kamati hiyo imewahakikishia wananchi kuwa maandalizi yote muhimu kwa ajili ya uchaguzi yamekamilika, na imewataka wakazi wa Tanga kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo kwa utulivu na nidhamu.
RC MAKALLA AZINDUA MSIMU WA SHEREHE ZA MILA ZA KIMASAI
JIJI LA DAR ES SALAAM NI SHWARI,JITOKEZENI KUPIGA KURA:RC CHALAMILA.
VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA WATANZANIA KUPIGA KURA KWA AMANI.
BODABODA NA MACHINGA HATUTAKUWA CHANZO KUVUNJA AMANI YETU
CWT YATOA WITO KWA WALIMU KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU NA KUELEIMISHA JAMII KUHUSU UMUHIMU WA KUPIGA KURA
PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
MKURANGA WAPO TAYARI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU KWA AMANI
Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya VSOMO ya VETA