CHALAMILA: WATAKAOJIZIMA DATA OKTOBA 29, TUTAWAFANYA NETWORK ZISOME | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

CHALAMILA: WATAKAOJIZIMA DATA OKTOBA 29, TUTAWAFANYA NETWORK ZISOME

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, amewataka wananchi wa Jiji hilo kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, akisisitiza kuwa hakuna tishio lolote la usalama litakalowazuia kutumia haki yao ya kikatiba.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
17 Oct 2025
CHALAMILA: WATAKAOJIZIMA DATA OKTOBA 29, TUTAWAFANYA NETWORK ZISOME

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, amewataka wananchi wa Jiji hilo kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, akisisitiza kuwa hakuna tishio lolote la usalama litakalowazuia kutumia haki yao ya kikatiba.

Akizungumza leo Ijumaa Oktoba 17, 2025, jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na makundi maalumu ikiwemo mama lishe, baba lishe, machinga, vijana na wadau mbalimbali wa maendeleo, Chalamila alisema Serikali imejipanga kuhakikisha kila mwananchi anapiga kura kwa amani na utulivu bila bughudha yoyote.

“Zoezi linaloendelea tarehe 29 mwezi huu, sisi Dar es Salaam tuna wapigakura waliojiandikisha milioni 4 laki 4 elfu 20 na mia 912. Mheshimiwa Waziri Mkuu, tunakuthibitishia kuwa wote watakaojitokeza kupiga kura hakuna jambo lolote baya litakalowakuta,” alisema.


Aidha, Chalamila aliwataka wananchi kupuuza makundi machache yanayotumia mitandao ya kijamii kusambaza taarifa za uchochezi, akisisitiza kuwa vyombo vya dola viko tayari kushughulikia uvunjifu wa amani.

Kwa kejeli iliyoamsha vicheko kutoka kwa hadhira, Mkuu huyo wa Mkoa alisema

“Wanaojizima data tutawawasha wenyewe, ili network ishike vizuri waone kinachoendelea. Sisi tunaitwa Wanachotaka, Tunataka!”


Kauli hiyo imeonekana kama ujumbe wa kuhamasisha wananchi kutoshawishika na hofu au propaganda za mitandaoni, bali wajitokeze kwa wingi kutumia haki zao.

Chalamila alisisitiza kuwa Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam iko imara katika kuhakikisha usalama wa wananchi wote kabla, wakati na baada ya uchaguzi huo, huku akiwataka wafanyabiashara wadogo kuendelea na shughuli zao kwa utulivu

"Amani tuliyonayo ni tunu kubwa. Hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuichezea. Ni wajibu wetu kuilinda,” aliongeza.

VIONGOZI WA DINI KATAVI WATOA KAULI "UCHAGUZI USITUGAWANYE"

VIONGOZI WA DINI KATAVI WATOA KAULI "UCHAGUZI USITUGAWANYE"

PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI

PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI

Dkt. Saada Mkuya: Uchaguzi Bila Vurugu Unawezekana, Bima Haziwezi Kulipa Madhara ya Kujitakia

Dkt. Saada Mkuya: Uchaguzi Bila Vurugu Unawezekana, Bima Haziwezi Kulipa Madhara ya Kujitakia

JWTZ YAWAHAKIKISHIA USALAMA WANANCHI, LIKIONYA KUHUSU UPOTOSHAJI MITANDAONI

JWTZ YAWAHAKIKISHIA USALAMA WANANCHI, LIKIONYA KUHUSU UPOTOSHAJI MITANDAONI

TUME YA UCHAGUZI YAONYA WANAOSHAWISHI KUTOPIGA KURA “NI KOSA KISHERIA’

TUME YA UCHAGUZI YAONYA WANAOSHAWISHI KUTOPIGA KURA “NI KOSA KISHERIA’