

Wakati Tanzania ikielekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwanamke na Nguvu ya Kijani, Dkt. Judith Mhina Spendi, ametoa wito wa kitaifa kwa Watanzania wote kusimama pamoja kulinda amani, umoja na mshikamano — nguzo kuu za ustawi wa taifa.
Wakati Tanzania ikielekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwanamke na Nguvu ya Kijani, Dkt. Judith Mhina Spendi, ametoa wito wa kitaifa kwa Watanzania wote kusimama pamoja kulinda amani, umoja na mshikamano — nguzo kuu za ustawi wa taifa.
Akizungumza kwa hamasa kubwa jijini Dar es Salaam, Dkt. Judith alitangaza kongamano la amani litakalofanyika kuanzia Oktoba 25 hadi 27 katika Viwanja vya Posta Kijitonyama, ambalo litawakutanisha viongozi wa dini, vijana, wanawake, wafanyabiashara, pamoja na taasisi za kijamii na serikali.
Dkt. Judith alisema kongamano hilo litakuwa jukwaa la kutafakari mustakabali wa taifa, hasa katika kipindi hiki ambacho macho ya dunia yote yameelekezwa Tanzania kuelekea uchaguzi huru, wa haki na wa amani.
“Tanzania imekuwa mfano wa kuigwa barani Afrika kutokana na utulivu wake. Amani ndiyo injini ya maendeleo; bila amani hakuna uwekezaji, hakuna elimu bora, hakuna huduma za afya zenye ubora. Hakuna taifa imara bila mshikamano,” alisema kwa msisitizo.
Aliongeza kuwa jukumu la kulinda amani si la viongozi pekee, bali ni wajibu wa kila Mtanzania — kuanzia kijijini hadi mijini.
“Tujifunze kusikilizana, kuheshimiana na kutofautiana kwa hoja, si kwa chuki. Uchaguzi ukipita, Tanzania inabaki ni yetu sote,” aliongeza.
Akihitimisha hotuba yake, Dkt. Judith alitoa kauli ya kugusa mioyo ya wengi kwa kusema:
“Mimi naahidi amani, wewe je?”
Kauli hiyo ilipokelewa kwa shangwe kutoka kwa washiriki waliokuwa ukumbini, wengi wakiahidi kuwa mabalozi wa amani katika jamii zao.
VIONGOZI WA DINI KATAVI WATOA KAULI "UCHAGUZI USITUGAWANYE"
WOTE WENYE HOMA ZA UCHAGUZI MSIKUBALI ZIKAPANDA KICHWANI, TUTAWADHIBITI- KANALI MTAMBI
PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI
CHALAMILA: WATAKAOJIZIMA DATA OKTOBA 29, TUTAWAFANYA NETWORK ZISOME
VIONGOZI WA KIMASAI WAAHIRISHA TOHARA KWA VIJANA 2,000 KUPISHA UCHAGUZI MKUU
PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
TUMEJIANDAA VYEMA KUDHIBITI UHALIFU NA WAHALIFU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU- POLISI
AMANI NDIYO UISLAMU, TUIHUBIRI NA KUILINDA- MUFTI ABUBAKAR