

Wananchi wa Mkuranga Mkoani Pwani wamesema wapo tayari kwa ushiriki wa uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 wakiwahimiza pia Vijana kutumia fursa hiyo na haki ya kikatiba ili kuchagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo kwa miaka mitano ijayo.
Wananchi wa Mkuranga Mkoani Pwani wamesema wapo tayari kwa ushiriki wa uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 wakiwahimiza pia Vijana kutumia fursa hiyo na haki ya kikatiba ili kuchagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo kwa miaka mitano ijayo.
Wananchi hao akiwemo Mzee Maulid Mwigange na Mariam Ngayonga wakati wakizungumza na Vyombo vya habari, wamewatoa wasiwasi wananchi na kuwaeleza kuwa Oktoba 29, 2025 kutakuwa na usalama na amani ya kutosha kutokana na namna ambavyo serikali imejipanga kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata nafasi kamili na usalama wa kushiriki kupiga kura.
"Tutachagua Kiongozi anayetufaa na tumehamasika kushiriki kwasababu ya maendeleo mengi tu tunayoyashuhudia Mkuranga ikiwemo stendi nzuri na hatubugudhiwi." Ameongeza kusema Mohamed Makame, mwananchi na mfanyabiashara mdogo wa Mkuranga.
Kwa upande wake Habiba Jasmin, Kijana na mjasiriamali mdogo wa Mkuranga ametoa wito wa Vijana kutumia vyema fursa ya upigaji kura kuamua kuhusu hatma yao ya miaka mitano ijayo, akiombea kheri uchaguzi huo ili ufanyike na umalizike kwa amani ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku za uchumi.
Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”
MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI
Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
Mkomi Awasisitiza Wakuu wa Taasisi Kusimamia Mifumo ya Kielektroniki Serikalini.
WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
TUMEJIANDAA VYEMA KUDHIBITI UHALIFU NA WAHALIFU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU- POLISI