MGOMBEA UDP ACHUKUA FOMU INEC ZA KUOMBA KUTEULIWA KUGOMBEA URAIS | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

MGOMBEA UDP ACHUKUA FOMU INEC ZA KUOMBA KUTEULIWA KUGOMBEA URAIS

Mgombea Urais wa Chama cha United Democratic Party (UDP), Saum Hussen Rashid, pamoja na mgombea mwenza Juma Hamis Faki, wamechukua rasmi fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama hicho.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
15 Aug 2025
MGOMBEA UDP ACHUKUA FOMU INEC ZA KUOMBA KUTEULIWA KUGOMBEA URAIS

Dodoma. Mgombea Urais wa Chama cha United Democratic Party (UDP), Saum Hussen Rashid, pamoja na mgombea mwenza Juma Hamis Faki, wamechukua rasmi fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama hicho.

Fomu hizo zimekabidhiwa leo Agosti 14, 2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele, katika hafla iliyofanyika makao makuu ya tume hiyo jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Saum ameishukuru INEC kwa mapokezi na utaratibu mzuri wa utoaji fomu, akibainisha kuwa chama chake kinaamini huu ni mwanzo wa uchaguzi huru na wa haki.

“Kama chama tumejipanga kuondoa changamoto zote kwenye jamii na kuwainua wananchi wanyonge, tunaamini Watanzania wanaweza kufanya maamuzi sahihi,” amesema.

Ameongeza kuwa vipaumbele vya UDP vinahusisha kuendelea kudumisha amani na utulivu vilivyoasisiwa na waasisi wa taifa, kutumia njia za amani kutatua migogoro, kuondoa ukatili wa kijinsia, na kuhakikisha rasilimali zote zinawanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

Kwa mujibu wa ratiba ya INEC, uteuzi wa wagombea wa nafasi ya Rais na Makamu wa Rais unatarajiwa kufanyika Agosti 27, 2025.

 

 

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAUDHUKUMU YAO HASA KATIKA KIPINDI HIKI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAUDHUKUMU YAO HASA KATIKA KIPINDI HIKI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

MGOMBEA NCCR MAGEUZI AJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI

MGOMBEA NCCR MAGEUZI AJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI

MPINA WA ACT WAZALENDO ACHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS

MPINA WA ACT WAZALENDO ACHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS

MLUYA WA CHAMA CHA DP ACHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS

MLUYA WA CHAMA CHA DP ACHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS

CUF WAMTUMA GOMBO KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS UCHAGUZI MKUU 2025

CUF WAMTUMA GOMBO KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS UCHAGUZI MKUU 2025