

Mgombea Urais wa Chama cha United Democratic Party (UDP), Saum Hussen Rashid, pamoja na mgombea mwenza Juma Hamis Faki, wamechukua rasmi fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama hicho.
Dodoma. Mgombea Urais wa Chama cha United Democratic Party (UDP), Saum Hussen Rashid, pamoja na mgombea mwenza Juma Hamis Faki, wamechukua rasmi fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama hicho.
Fomu hizo zimekabidhiwa leo Agosti 14, 2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele, katika hafla iliyofanyika makao makuu ya tume hiyo jijini Dodoma.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Saum ameishukuru INEC kwa mapokezi na utaratibu mzuri wa utoaji fomu, akibainisha kuwa chama chake kinaamini huu ni mwanzo wa uchaguzi huru na wa haki.
“Kama chama tumejipanga kuondoa changamoto zote kwenye jamii na kuwainua wananchi wanyonge, tunaamini Watanzania wanaweza kufanya maamuzi sahihi,” amesema.
Ameongeza kuwa vipaumbele vya UDP vinahusisha kuendelea kudumisha amani na utulivu vilivyoasisiwa na waasisi wa taifa, kutumia njia za amani kutatua migogoro, kuondoa ukatili wa kijinsia, na kuhakikisha rasilimali zote zinawanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.
Kwa mujibu wa ratiba ya INEC, uteuzi wa wagombea wa nafasi ya Rais na Makamu wa Rais unatarajiwa kufanyika Agosti 27, 2025.
WATANZANIA WAASWA KUJITAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO.
TUKITUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA TUTAOKOA HEKTA 400,000 ZA MISITU ZINAZOTEKETEA KWA MWAKA-MJIOLOJIA NSAJIGWA.
MHANDISI SANGA AONGEZA MWEZI MMOJA KLINIKI YA ARDHI KIVULE KUONGEZA KASI YA UTOAJI HATI
SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA FURSA, KWA WAKULIMA WA MWANI TANGA
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAUDHUKUMU YAO HASA KATIKA KIPINDI HIKI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Serikali Inaendelea Kuimarisha Mazingira Kuwawezesha Vijana Kuanzisha Shughuli Za Uzalishaji Mali.
NGO's zatakiwa Kuwa Mawakala wa mabadiliko chanya katika Jamii.
INEC YAMKABIDHI FOMU ZA UTEUZI MGOMBEA URAIS WA CHAMA CHA NLD DOYO HASSAN DOYO
MGOMBEA KITI CHA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA NRA ACHUKUA FOMU TUME
KADEGE WA CHAMA CHA UPDP ACHUKUA FOMU ZA URAIS