

Nishati ya gesi asilia imekuwa na Mchango mkubwa Kwa nchi hasa kwenye Sekta ya umeme ambapo Serikali imewekeza kwenye bwawa la umeme hii ni nishati muhimu
Nasasa gesi hii ni muhimu Kwa Matumizi ya majumbani viwandani na magari nasasa upo mpango gesi hii itumike zaidi kwenye magari na maeneo mengine ya nchi Kwa gesi hiyo imekuwa ikipatika Mtwara Lindi na Dar es salam
Hayo yameelezwa Leo na Charles Nyangi Mkuu wa kitengo cha ushirikishwaji wa wazawa na ushirikishwaji wa ndani kutoka Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ufunguzi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 yaliyofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Ameongeza kuwa gesi hii itafika katika mikoa mingine kadri wananchi watakavyoielewa na kuona umuhimu wake Kwa kurahisisha na kuhimiza Matumizi ya nishati safi.
Aidha amesema Wapo kwenye Maonesho hayo kuwaelezea Wananchi kuhusu shughuli zinazofanywa na Mamlaka hiyo pamoja na fursa zinazokuwepo katika shughuli za Mkondo wa juu wa Petroli
PURA ilianzishwa chini ya Sheria ya Petroli mwaka 2015 na moja la jukumu lilipoewa ni kuhamasisha ushiriki wa wawazawa katoka shughuli za Mkondo wa juu wa Petroli.
Amesema ushiriki huo umegawanywa katikati makundi matatu ambayo ni Kupitia ajira,kupitia ujasiriamali kwa maana ya kununua na kusambaza Bidhaa au uwekezaji.
" Hivyo tunapokuwa katika Maonesho haya ni kuwaelezea Wananchi majukumu na shughuli zinazopatikana kwenye mkono ," amesema
PURA ina matumaini kuwa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, wawekezaji watakuwa wamepatikana, jambo ambalo litaleta manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Sanjari na hayo PURA inafanya kazi ya Kuwajengea uwezo watanzania na kampuni za Kitanzania kushiriki kikamilifu katika miradi ya utafutaji,uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika shughuli za mafuta na gesi asilia nchini.
Maadhimisho hayo yamebeba kauli mbiu isemayo "Himiza Matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji"
BODI YA MKONGE TANZANIA YATANGAZA FURSA KWA WATANZANIA.
SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.
DCEA:SERIKALI IMEPUNGUZA KASI YA WALAIBU WA DAWA ZA KULEVYA.
ULINZI NA USALAMA BAHARINI UMEIMARIKA;TASAC
VITONGOJI VYOTE 64,359 VITAKUWA NA UMEME IFIKAPO 2030
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.
Mkoa wa Katavi umeendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM)
UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.
AMANZI NA BABU TALE USO KWA USO JIMBONI