AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Michezo

AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.

Waheshimiwa Wabunge, Watumishi wa Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Watumishi wa Benki ya Azania ,Viongozi wa Shirikisho la Mpira nchini, Viongozi wa Klabu za Simba na Yanga, pamoja na wananchi mbalimbali wameshiriki kwenye Azania Benki Bunge Bonanza ambalo limeshirikisha Mashabiki wa Timu za Simba na Yanga na kuongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa

moreen Rojas (Dodoma)
By moreen Rojas (Dodoma)
04 Feb 2025
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.

Akizungumza katika bonanza hilo liliofanyika februari mosi,2025 katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlin jijini Dodoma Mhe.Majaliwa amesema Serikali imejipanga vyema kukamilisha maandalizi muhimu kwa ajili ya Michuano ya Mpira wa Miguu kwa Nchi za Africa CHAN na AFCON.

"Tanzania imejipanga vizuri, kuhakikisha kuwa michuano hii inafanyika hapa Nchini, Serikali inawajibika kuhakikisha inaandaa viwanja na miundombinu mingine."

Amesema kuwa tayari ukaguzi wa baadhi ya viwanja umefanyika na vimeonekana kukidhi vigezo “Viwanja vilivyokaguliwa vipo Tanzania bara na Visiwani, na kazi bado inaendelea, lengo ni kuhakikisha michuano hii inafanyika kwa ufanisi”

Amwongeza kuwa amesema ni vyema sasa Watanzania wakajipanga kutumia fursa zitakazo jitokeza kutokana na kuwepo kwa michuano hiyo hapa Nchini.

Aidha, ametoa Ponhezi Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson kwa kuandaa Tamasha la Michezo la Bunge Bonanza ambalo limewakutanisha wabunge na wanamichezo mbalimbali wa Mkoani Dodoma.

Aidha ametoa Rai  kwa  Watanzania kuendelea na utamaduni wa kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao.

Bonanza hilo lilianza kwa matembezi kutoka eneo la Chuo cha Mipango hadi katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlini iliyopo Jijini Dodoma ambapo mashindano ya michezo mbalimbali kati ya Mashabiki wa Simba na Yanga yamefanyika.

"Kiukweli tumefurahi benki ya AZANIA kutuleta pamoja wanamichezo kwani inajenga undugu na kuimarisha afya zetu pamoja na kuhamasisha  umuhimu wa mazoezi Kwa jamii ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukizwa"Amesema Khadija Juma mmoja wa washiriki wa bonanza hilo ambaye ni shabiki wa Simba.

Naye Adam Peter ambaye ni shabiki wa yanga amesema kitendo walichokifanya AZANIA benki ni kitendo kizuri na Cha kuigwa na benki nyingine ikiwa ni kuhakikisha tunakuwa na jamii nzuriii inayopenda kulinda afya zao kupitia mazoezi.

MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.

MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.

DAR CITY YAING’ARISHA TANZANIA MASHINDANO YA KIKAPU AFRIKA MASHARIKI

DAR CITY YAING’ARISHA TANZANIA MASHINDANO YA KIKAPU AFRIKA MASHARIKI

Ndaisaba azidi kumwaga  Fedha katika sekta ya Michezo Wilayani Ngara

Ndaisaba azidi kumwaga Fedha katika sekta ya Michezo Wilayani Ngara

MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR ATAKA KANUNI NA MAADILI MICHEZONI ZIWEKWE ILI KUONDOA MITIZAMO HASI.

MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR ATAKA KANUNI NA MAADILI MICHEZONI ZIWEKWE ILI KUONDOA MITIZAMO HASI.