MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR ATAKA KANUNI NA MAADILI MICHEZONI ZIWEKWE ILI KUONDOA MITIZAMO HASI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Michezo

MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR ATAKA KANUNI NA MAADILI MICHEZONI ZIWEKWE ILI KUONDOA MITIZAMO HASI.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Mhe. Othman Massoud Othman amevitaka vikundi vya mazoezi nchini kuweka kanuni na miongozo ya maadili ambayo itasaidia kuondoa mitizamo hasi kwa jamii juu ya ushiriki wa makundi yote katika vikundi vya mazoezi na michezo.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
28 Jul 2024
MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR ATAKA KANUNI NA MAADILI MICHEZONI ZIWEKWE ILI KUONDOA MITIZAMO HASI.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Mhe. Othman Massoud Othman amevitaka vikundi vya mazoezi nchini kuweka kanuni na miongozo ya maadili ambayo itasaidia kuondoa mitizamo hasi kwa jamii juu ya ushiriki wa makundi yote katika vikundi vya mazoezi na michezo.

Ametoa wito huo wakati akizungumza na vikundi vya mazoezi katika halfa ya kuhamasisha ushiriki wa jinsia zote kwenye mazoezi na michezo ikiwa ni  maadhimisho ya kutimia miaka kumi ya klabu ya mazoezi Gombani kisiwani Pemba.

Amesema, kuwepo kwa kanuni zinazosimamia maadili katika mazoezi na michezo kutasaidia watu wengi hasa wanawake kuona eneo hilo ni salama kwao na kuondoa dhana potofu iliyojengeka katika jamii.

Ameeleza, "niwaombe tuweke kanuni za kusiamamia maadili zitakazo ondoa dhana potofu kwa jamii ili tuweze kuwavutia watu wengi kushiriki mazoezi kwasababu hili jambo ni jema zaidi."

Aidha, makamu huyo wa kwanza wa Rais ambaye aliongoza matembezi na mazoezi ya wanamichezo hao alifahamisha kuwa taifa linapata hasara kubwa kugharamia matibabu ya maradhi yasiyoambukiza yanayosababishwa na mfumo wa maisha ambapo iwapo jamii itakuwa na mwamko wa kushiriki katika mazoezi na michezo itasaidia kupunguza gharama hizo.

"Jambo hili ambalo mnaliendeleza kwetu sisi wengine linatupa faraja sana kwasababu tunajua mnafanya jambo kubwa kwa jamii na nchi yetu kwani kama kuna jambo ambalo nchi inapata hasara ni kwenye matibabu. Na matibabu ya maradhi yasiyoambukiza kwahakika ni ya ghali sana na nyinyi nyote ni mashahidi," alieleza, Mhe. Othman Masoud.

Katika hatua nyingine alihimiza jamii kupewa elimu ya matumizi lishe ili kujiepusha na ulaji holela unaopelekea athari kiafya.

Mhe. Othman Masoud alisema, “twende mbali zaidi kutoa ya elimu ya lishe kwa jamii. Kwasababu hili wengi bado huko tuna tatizo. Tumeacha sasahivi vyakula asilia. Mwingine anaona pengine vyakula asilia sio usasa. Lazima twende katika hatua ya kujitunza na kujipenda kwa kutambua kipi kibaya na kipi kizuri cha kula.”

Naye Mkuu wa wilaya ya Chake chake, Abdalla Rashid amemshukuru Mhe. Othman kwa kuwa miongoni mwa washiriki katika bonanza hilo na kuwahimiza wananchi kuhakikisha kwamba wanahamasishana ili wajenge utamaduni wa kufanya mazoezi katika kujiepusha na maradhi mbalimbali yasiyoambukiza.

Akitoa salamu za wadau, afisa programu ya michezo kwa maendeleo kutoka Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Khairat Haji alieleza bado kuna changamoto kwenye jamii ya uelewa kuhusu umuhimu wa mazoezi na kupelekea vikwazo kwa makundi yote hasa wanawake kushiriki kikamilifu katika mazoezi na michezo.

Aidha aliongeza, ukosefu wa miundombinu na vifaa wezeshi vya mazoezi ni kikwazo katika ufikiaji wa usawa wa kijinsia kkwenye michezo na kuomba serikali na wadau kusaidia kuboresha miundombinu hiyo ili kuwezesha kila mmoja kushiriki bila kikwazo.

"Kuna changamoto kadhaa ambazo tumeziona ikiwemo ukosefu wa vifaa na miundombinu wezeshi kwaajili ya makundi yote kushiriki katika michezo mbalimbali," alifahamisha afisa huyo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa klabu ya mazoezi Gombani, Hamad Malengo aliomba wadau kuungana pamoja kushiriki katika michezo na mazoezi ili kuondoa dhana hiyo potofu iliyojengeka katika jamii kuwa kushiriki michezo ni kujifunza uhuni.

Alisema, "elimu kwa jamii inahitajika zaidi ili kutoa mwamko wa watu kushiriki kwenye mazoezi na kuachana na dhana kwamba michezo ni uhuni. Ni lazima tusimame pamoja ili kila mmoja wetu aweze kushiriki mazoezi kwaajili ya afya yake.”

Hafla hiyo ya kuhamasisha ushiriki wa jinsia zote kwenye mazoezi na michezo ikiwa ni maadhimisho ya kutimia miaka kumi ya klabu ya mazoezi Gombani kisiwani Pemba iliyoandaliwa kwa kushirikiana na TAMWA-ZNZ na Shirika ka Bima la Zanzibar  imevishirikisha vilabu zaidi ya vitano vya mazoezi kutoka Unguja, Tanga na wenyeji Pemba.

BONAZA LA MICHEZO KUFANYIKA JULAI 20-28 PEMBA.

BONAZA LA MICHEZO KUFANYIKA JULAI 20-28 PEMBA.

NDOTO YA LEBRON JAMES YA KUCHEZA NA MWANAE TIMU MOJA YATIMIA BADO YA RONALDO NA MWANAE

NDOTO YA LEBRON JAMES YA KUCHEZA NA MWANAE TIMU MOJA YATIMIA BADO YA RONALDO NA MWANAE

TIMU ya mahakama mpira wa miguu yaibuka na ushindi dhidi ya timu ya Bunge.

TIMU ya mahakama mpira wa miguu yaibuka na ushindi dhidi ya timu ya Bunge.

Mavunde awavuta nyota wa Yanga, Ujirani mwema ndondo Cup Dodoma

Mavunde awavuta nyota wa Yanga, Ujirani mwema ndondo Cup Dodoma